WATAALAMU WA UDHIBITI WA CHAKULA NA DAWA BANDIA WAKUTANA

 
Wataalamu wa vyombo vya udhibiti wa vyakula na dawa feki katika nchi 16 mashariki na kusini mwa Afrika wamekutana jijini Dar es Salaam kujadili changamoto na kuweka mfumo wa pamoja chini ya uratibu wa shirika la afya duniani unaolenga kuliepusha bara la Afrika kugeuzwa dampo la bidhaa feki duniani.
Kwa mujibu wa taarifa ya meneja wa mradi wa udhibiti kutoka makao makuu ya shirika la afya duniani yaliyopo Geniva nchini uswis Bw. Michale Deats amesema mkutano huo wa siku tatu mbali na kujadili changamoto za udhibiti pia mkutano huo utaweka mikakati shirikishi ya kuhakikisha Afrika inafunga njia zote za uingizaji bidhaa za aina hiyo kwa usalama wa afya za binadamu huku akifafanua tatizo hilo na hatua za udhibiti katika eneo la Afrika na dunia kwa ujumla.
Awali katika taarifa ya mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya chakula a dawa nchini tfda bw. Hiit sillo pamoja na kueleza hatua za mamlaka katika udhibiti alipongeza shirika la afya duniani who kwa kuiteuwa tanzania kuwa mwenyeji wa mkutano huo muhimu akieleza fulsa hiyo kuchochea mikakati ya mamlaka na taifa katika kudhibiti uingizaji wa vyakula na dawa vilivyopo chini ya kiwago.
Mkutano huo ulifunguliwa na naibu waziri wa afya na ustawi wa jamii dk. Seifu rashidi akijipambanua kuchukua hatua kali dhidi ya wanaokiuka taratibu na wakati huo akijikuta katika wakati mgumu kujibu maswaili ya waandishi wa habari yaliyomtaka kueleza hatua zilizochukuliwa dhidi ya mmiliki wa kiwanda kilichothibitika kutengeneza Arv feki na kuelekeza lawama zake kwa mkurugenzi wa mashtaka dpp anayemtaja kutambua wajibu wake.
NA ITV


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo