VIFUSI VILIVYOLUNDIKWA BARABARA YA SUNJI - LUPILA WILAYANI MAKETE VYAKERA WAFANYABIASHARA

 Vifusi hivyo vikiwa barabarani
 Greda likianza kusambaza vifusi hivyo jana saa 10 jioni.

Ukaaji wa vifusi vilivyolundikwa katika barabara ya Sunji – Lupila kwa takribani mwezi mmoja bila kusambazwa umelalamikiwa na wafanyabiashara waliofika mnadani Lupila wilayani Makete mkoani Njombe kutokana na kupata adha kubwa wakati wakisafirisha bidhaa zao

Hayo yamesemwa na wafanyabiashara hao wakati wakizungumza na waandishi wa habari mnadani hapo na kuitaka serikali kulirekebisha hilo mapema ili iwe rahisi kwao kuleta tena bidhaa mwezi ujao

Mfanyabiashara wa mitumba Mama Mwalukisa amesema kutokana na wao kutumia magari makubwa kusafirisha bidhaa hizo, magari hayo yammewapa tabu kubwa barabarani kutokana na kukwama kwenye vifusi hivyo ilihali huu si msimu wa masika

“Yaani kwa kweli kama tungejua barabara iko hivi hata tusingekuja, magari haya tumekodi halafu tunajua barabara ni nzuri lakini kwa hali hii kwa kweli hapana, tunatoa wito kwa serikali irekebishe hii barabara kabla yam nada ujao wa mwezi Augusti kama wanataka tuje tena” alisema Mama Mwalukisa

Amesema kutokana na magari hayo kukwama mara kwa mara kwenye vifusi na wakati mwingine gari kulala, kumemwogopeha na kuzaimika kuteremka na kupanda kwenye gari la abiria ili kuondokana na kero ya kuhofu mara kwa mara

Naye mwenyekiti wa wafanyabiashara mkoa wa Njombe ambaye alikuwepo mnadani hapo Bi Nesfaneti Digati amesema ni muda wa serikali kutatua kero hiyo mara moja kwa kuwa lengo la wafanyabiashara hao ni kuleta huduma kwa wananchi tena kwa bei nafuu

Akizungumzia kero hiyo diwani wa viti maalumu tarafa ya Ukwama (kata ya Lupila ikiwemo) Bi Lenesta Lwila amekiri kuwepo kwa kero hiyo na kusema wao kama madiwani wamemwagiza mhandisi wa wilaya kuona uharaka wa kusambaza vifusi hivyo, lakini kabla ya kufanya hivyo greda la halmashauri ambalo lingetumika kwa kazi hiyo limeharibika na lipo katika matengenezo

Amesema mbali na hivyo wanawasiliana na mhandisi kuona nini wakifanye ili kutatua tatizo hilo na anaimani kuwa vitasambazwa kabla ya mnada ujao na wakija tena mara nyingine watakuta barabara iko safi

Hata hivyo mtandao huu umekuta zoezi la kusambaza vifusi kuanzia Maliwa hadi Lupila ukianza, ambapo mwandishi wetu ameshuhudia usambazaji wa vifusi ukuanzia Maliwa


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo