HALMASHAURI YA WILAYA YA MAKETE YAPONGEZWA KWA KUANZISHA MNADA LUPILA

Wananchi wa kata ya Lupila wilayani Makete mkoani Njombe, wameipongeza halmashauri ya wilaya ya Makete kwa kuanzisha kwa mara ya kwanza mnada katika kata hiyo ambao umewaletea unafuu wa bei za mahitaji mbalimbali waliyoyapata mnadani hapo

Wakizungumza na mwandishi wetu wananchi hao wamesema kwa mara ya kwanza mnada huo kufanyika katani hapo, ambapo wengi wao wamejipatia mahitaji mbalimbali ambayo walikuwa wakiyafuata mbali na kulazimika kununua kwa bei kubwa

Bw. Aldo Sanga amesema bidhaa kama nguo walikuwa wakienda kuzinunua Ikonda ama mkoani Njombe umbali wa zaidi ya kilomita 50 na hivyo kulazimika kulipa nauli kubwa lakini kunapokuwepo na mnada bei hupungua

“Mfano hapa Lupila mche wa sabuni huuzwa shilingi 1500 kwenye maduka lakini leo nimenunua hapa mnadani kwa sh. 1000 kwa mche mmoja, sasa huu si unafuu kwetu

Kwa upande wao wafanyabishara wameitaka halmashauri ya wilaya ya Makete kuongeza kasi ya kutangaza minada hiyo kupitia vyombo vya habari na viongozi mbalimbali ili taarifa ziwafikie wananchi wote na waongezeke zaidi ya waliofika jana

Mama Mwalukisa ni mfanyabiashara aliyekuwa mnadani hapo ambapo amesema ingawa wananchi walikuwa wengi kiasi mnadani hapo lakini wamebaini kuwa taarifa hazikufika ipasavyo kwa wananchi lakini pia kutokana na mnada huo kufanyika kwa mara ya kwanza eneo hilo huwenda nayo imechangia watu kutoshiriki kwa wingi

Akizungumzia suala hilo afisa biashara wilaya ya Makete Bw. Edonia Mahenge amesema wao walitangaza matangazo hayo redioni pamoja na kwenye nyumba za ibaada lakini pia hawataacha na badala yake wataongeza kasi ya matangazo ili taarifa ziwafikie wananchi wote


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo