WATOTO WAPUNGUZA KASI YA UUWAJI WA MBWA WANAOZAGAA OVYO MITAANI

MTAALAMU ALIYETEULIWA KUUWA MBWA WANAOZAGAA WILAYANI BUKOMBE MR.MAGAI MKAMA AKIENDELEA KUTOA DOZI KWA MMBWA WANAOZAGAA MJINI USHIROMBO.
 
GEITA
Zoezi la kuuwa mbwa wanaozagaa ovyo  ambao wanadhaniwa kuwa na kichaa cha mbwa wilayani Bukombe mkoani Geita,huwenda likachelewa kukamilika kutokana na changamoto ya watoto kujaa katika maeneo yanayofanyika mauaji hayo.
 
Mratibu wa zoezi hilo Dr.Sosthenes Nkombe amesema kuwa watoto wilayani humo wamekuwa ni kikwazo cha ufanisi wa zoezi hilo kutokana na kujaa katika maeneo ya tukio hali ambayo ni hatari kwa uhai wa watoto hao.
 
Nkombe amesema watoto wamekuwa kikwazo kwa sababu wanasimama mbele ya mdomo wa bunduki ambayo inatumika kuulia mbwa hao hali inayowalazimu kuwafukuza kwanza kitendo kinachowafanya  mbwa hao kukimbia.
 
Akiendelea kufafanua Nkombe amesema kuwa changamoto nyingine ni wananchi kutoelewa maana ya kichaa cha mbwa na madhara yake pamoja na kufuga mbwa bila kuwapa matibabu ikiwemo chanjo.
 
Katika hatua nyingine Nkombe amewashukuru wananchi kwa ushirikiano wanaoutoa ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa za mahali walipo mbwa na kuwataka wazazi na walimu kuwakataza watoto kusimama katika maeneo ambayo zoezi hilo linaendelea.
 
Kwa upande wao baadhi ya wananchi wa wilaya ya Bukombe wameishukuru halmashauri kwa kutekeleza zoezi hilo na kwamba mbwa hao wamekuwa tishio sana hususan kwa watoto wadogo.
 
Zoezi la kuuwa mmbwa wanaozagaa linatarajia kuendelea katika maeneo ya Lunzewe,Masumbwe na Lulembela ambapo kwa mji wa ushirombo mpaka sasa zaidi ya mbwa 214 wameuwawa.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo