WATOTO MAKETE WAOMBA MSAADA WA SERIKALI KUDHIBITI WAZAZI NA WALEZI WANAOJIHUSISHA KIMAPENZI NA WATOTO

Umati wa watoto wa kata ya Ipelele waliofurika kwenye maadhimisho ya siku ya mtoto wa afrika
Mgeni rasmi ambaye ni mkuu wa wilaya ya Makete Josephine Matiro akihutubia wananchi waliofika kumsikiliza
======

Wazazi na walezi wanaojihusisha kimapenzi na watoto wametakiwa kuacha vitendo hivyo mara moja na badala yake watumie muda huo wanaoutumia kuwarubuni kuwafundisha watoto hao stadi za maisha ikiwemo namna ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya UKIMWI pamoja na kuzingatia masomo yao shuleni

Sanjari na hayo kina mama wengi ambao pia wanafumbia macho vitendo vya unyanyasaji na ukatili wanavyofanyiwa watoto kuacha mara moja kwa kuwa mkono wa sheria hautawaacha pindi watakapobainika

Kauli hiyo imetolewa na mgeni rasmi ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Makete Mh. Josephine Matiro katika hotuba yake aliyoitoa kwenye maadhimisho ya siku ya mtoto wa afrika ambayo kiwilaya yameadhimishwa katika kata ya Ipelele tarafa ya Magoma wilayani hapo

Mbali na hayo pia mh Matiro amekemea tabia inayoendekezwa na baadhi ya wazazi na walezi hivi sasa ya kwenda na watoto sehemu za starehe hasa vilabuni kwa kuwa tabia hiyo inawajengea watoto hao mazingira na tabia mbaya hapo baadaye huku akiagiza viongozi na mamlaka husika kuchukua hatua dhidi ya wazazi na walezi wanaofanya hivyo

“Kwa kweli hii ni aibu kubwa hivi vitu kama hivi ni mpaka tukemewe kwani hamuono kama hamtendi haki kwa watoto? Sote tunajua wazazi wakiwa vilabuni tena wakiwa wamelewa mambo wanayofanya kwa kweli hayajengi na wale watoto wanashuhudia, baadaye wakikua wanaanza kufanya hivyo hivyo, hivi tunajenga taifa gani?”amesema Matiro

Amesema hivi sasa wazazi na walezi wanatakiwa kuwa karibu na watoto wao kwa kuwa watoto wanahitaji ukaribu kutoka kwao pamoja na kuwa na moyo wa kusaidia watoto yatima na si kuyaachia mashirika pekee kwa kuwa muda wowote pasipo taarifa suala ya uyatima linaweza kuikumba familia yako

Awali mtoto Alpani Abdani akisoma risala kwa niaba ya watoto wa wilaya ya Makete walimwaomba mkuu wa wilaya kukemea vitendo vinavyofanywa na baadhi ya wazazi na walezi kwa kkwenda na watoto vilabuni ama baa pamoja na wale wanaojihusiha kimapenzi na watoto kwani vitendo hivyo ni hatari ikiwemo watoto kupata maambukizi ya virusi vya Ukimwi

Katika maadhimisho hayo watoto wapatao 60 wanaoishi katika mazingira hatarishi ambao wanatoka kwenye vijiji vya kata ya Ipelele walikabidhiwa zawadi za madaftari na kalamu

Katika wilaya ya Makete jumla ya watoto yatima 42,628  ambapo kati yao 6,745 wanaishi katika mazingira hatarishi


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo