TCRA YATOA SEMINA JUU YA SHERIA YA MAWASILIANO KWA WADAU WAKE IRINGA

Mamlaka ya mawasiliano Tanzania wametoa semina juu ya sheria ya mawasiliano na mfumo mpya wa leseni  kwa wadau mbalimbali pamoja na aina za leseni.

Akizungumza Mkurugenzi wa mawasiliano wa  idara ya sheria  Bi ELIZABETH NZANG katika semina hiyo iliyofanyika katika chuo kikuu huria Manispaa ya Iringa, amesema kuwa mamlaka inahimiza wadau wote waliochukua leseni na watakaoomba leseni kufuata sheria kwani kwa kutofanya hivyo mamlaka itamtoza faini , itamfungia kituo au adhabu ya kifungo.

NZANGI amesema kuwa ukiukwaji wa sheria mamlaka inayo wajibu kuwaadhibu huku akitaja aina za leseni kuwa kumiliki na kujenga miundombinu, kuendesha na kuunganisha mawasiliano,kutoa huduma za masiliano ,leseni za maudhui , vifaa vya mawasiliano, leseni za very small aperture terminals pamoja na utumiaji wa vifaa vya masafa.

Mbali na suala hilo la leseni mamlaka pia inatoa taarifa kuanzia july mosi yeyote ambaye atanunua simu ambayo haijasajiliwa haitotumika na kusema kuwa unaposajiliwa hakikisha kwa namba inayianzia  nyota mia na sita leri ili kuhakikisha kama usajili umekamilika.

Aidha Mamlaka inaomba wananchi kutoa ushirikiano ili waweza kufanya kazi vizuri kwa mujibu wa sheria namba 21 huku ikiwaonya watanzania kutonunua simu kwa wamachinga na kuahidi kushughulikia malalamiko kwa haraka likiwemo la utumiaji wa mabadiliko ya fedha .


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo