DIWANI AKIRI WAZI TATIZO LA MAJI KWENYE KATA YAKE,WANANCHI WAMTUPIA LAWAMA.

Kutokana na kukitihiri kwa kero ya maji katika kata ya Nduli maeneo ya njia panda ya Mgongo Manispaa ya Iringa, wananchi wameutupia lawama uongozi wa kata hiyo kwa ukosefu wa huduma kwa kipindi kirefu.

Wakizungumza na mapema leo,wakazi hao wa kata ya NDULI maeneo ya njia panda ya Mgongo, wamesema kuwa inawalazimu kutumia maji ya madimbwi kwa miaka mingi na tayari michango kwa ajili ya kuleta huduma hiyo ya maji imekwisha changwa.

Akijibia lawama hizo Diwani wa kata ya nduli mh. Rashidi Chonanga amekiri kuwepo kwa tatizo la maji katika kata yake na sasa wanamtafuta mkandarasi wa maji ili kuhakikisha maji yanafika maeneo yote ya Nduli.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo