POLISI IRINGA YASHIKILIA WATU 7 KWA TUHUMA ZA UCHOCHEZI


Watu saba wanashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za  kufanya fujo katika chaguzi ndogo za udiwani katika wilaya ya kilolo na mufindi huku likimshikilia  mtu mmoja aitwaye Saadat Daud kwa kosa la uchochezi.
 
Akizungumza na wandishi wa habari kamanda wa polisi mkoa wa Iringa,Ramadhani Mungi, mnamo tarehe 15 mwezi huu majira ya saa 7 mchana katika kijiji cha ng’ang’ange wilaya ya kilolo Runyiliko Nyaulingo (60) alifika katika eneo la CCM,wakifamya maandalizi ya mkutano wa kampeni na kuwafanyia fujo.
 
Kamanda amesema kufuatia fujo hizo wafuasi wa ccm walimpiga na kumjeruhi mkono kitendo kilichopelekea wafuasi wa CHADEMA wakiwa na marungu na mapanga walikwenda kumuokoa mwenzao lakini polisi waliwahi kufika kutuliza fujo na wanamshikilia WILHADI NGOGO 40 inasemekana kuwa ni mfuasi wa chadema.
Kamanda pia majira ya saa 5 wafuasi wa chadema walikuwa wakifanya kampeni za nyumba kwa nyumba walifika katika kijiji cha  maguvani kwenye nyumba ya LUSTIKA MHELELE gafla walifika watu wanaodhaniwa kuwa ni wafuasi wa ccm na kumshambulia kwa kitu chenye ncha kali DANIEL EDSON 45 na katika tukio hilo wanamshikilia YOHANES MCHAFU 45.
Amesema kuwa baada ya kujeruhiwa kwa DANIEL EDSON wafuasi wa chadema walifunga barabara ya mbeya iringa kwa magogo wakiongozwa na kiongozi wao aitwaye SAADAT DAUD na fujo hizo zilitulizwa na jeshi la polisi.
Aidha ameongeza kwa kusema kuwa mnamo tarehe 16 majira ya saa 11 jioni waliwakamata watu watatu wafuasi wa chadema wakiwa na mapanga na misumari katika kijiji cha ukemele kata ya mbalamaziwa DAMIANI OMARI 18 amemaliza kidato cha nne katika shule ya sekondari sangu mkoani mbeya JOSEPH MWAKATO 17 mwanafunzi kidato cha pili sinde sekondari pamoja na GEORGE MYAO 32 mpishi wa tazara ambaye pia ni katibu wa BAVICHA.
 
CREDITS:JIACHIE


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo