MKUU WA WILAYA YA MAKETE AJITOLEA KUWASAIDIA SARE ZA SHULE WATOTO YATIMA WAWILI

Jitihada zinazofanywa na asasi ya ELCT Makete kupitia program yake ya Pamoja Tuwalee zimeendelea kuzaa matunda baada ya hivi karibuni kuwaibua watoto wawlili wa kata ya Ipelele wilayani Makete ambao wanaishi katika mazingira hatarishi zaidi na kuweka matatizo yao kwa jamii ili iwasaidie

Jitihada hizo zilizaa matunda kwa watoto hao Zaifa Daudi na Nobi Sadiki (PICHANI JUU) ambapo mkuu wa wilaya ya makete Bi Josephine Matiro ameahidi kuwasaidia watoto hao sare za shule kwa kipindi chote atakachokuwepo kwenye wilaya hiyo

“Ndugu zangu nimeguswa sana na maelezo ya watoto hao ambao wanaishi katika mazingira hatarishi, wanadiriki kufanya vibarua ili wazilee familia zao ukizingatia watoto hawa ni yatima, mimi naomba suala la uniform (sare) za hawa watoto niulizwe mimi mpaka nitakapotoka Makete

Kwa mujibu wa Mratibu wa program ya pamoja Tuwalee wilayani hapo Mchungaji Ezekiel Sanga, watoto hao mmoja wao anasoma darasa la tatu na amamlea bibi yake ambaye ni mzee sana ambapo mtoto huyo hulazimika kutafuta vibarua na kuvifanya ili apate fedha za kujikimu yeye na bibi yake huku mtoto mwenzake naye akishirikiana na dada yake kufanya vibarua ili wajikimu kumaisha

Mchungaji Sanga amesema pamoja na ukosefu wa sare za shule walionao watoto hao lakini pia malazi yao ni tabu, na wakati mwingine wanashindwa kuhudhuria masomo yao kwa kuwa hulazimika kwenda kutafuta vibarua vya kufanya huku akiitaka jamii inayowazunguka watoto hao kuona umuhimu wa kuwasaidia kwani watoto hao hawakupenda kuishi maisha hayo magumu waliyonayo mara baada ya kufiwa na wazazi wao

Hivi majuzi wakati wa maadhimisho ya siku ya mtoto wa afrika watoto hao walichangiwa zaidi ya sh. 282,500 lakini pia hamasa ikawekwa kwa jamii inayowazunguka watoto hao kuwasaidia kwa mahitaji yao ili watoto hao waishi kwa raha

Programa hiyo ya pamoja tuwalee wilayani hapo imekuwa ikiibua changamoto wanazokumbana watoto na kuziweka wazi ikiwemo kuwatafutia ufumbuzi wa matatizo yanayowakumba watoto hao kwa kuwashirikisha wadau kuona matatizo hayo ni ya kila mtu

Na Edwin Moshi


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo