MKUU WA WILAYA YA BAGAMOYO AAGIZA WATOTO WALINDWE

MKUU wa Wilaya ya  Bagamoyo, mkoani Pwani, Ahmed Kipozi ameitaka jamii kuhakikisha inashughulikia suala la kuwalinda watoto ikiwemo suala la ukatili, mila kandamizi na utumikishaji usiofaa.

Kipozi alisema hayo jana jumapili alipokuwa mgeni rasmi wakati wa maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika inayofanyika kila mwaka Juni 16.

Akihutubia wananchi, pamoja na watoto wakiwemo  kutoka shule mbalimbali za msingi za Wilaya hiyo, alisema kuwa Jamii inajukumu kubwa ya kuakikisha suala la ulinzi linatekelezwa kwa pamoja hasa katika kumlinda mtoto.

“Kumlinda mtoto na mila kandamizi ni jukumu letu, nasi hatuna budi kuwahakikishia hilo pamoja na kutokomeza vitendo viovu dhidi yao” alisema Kipozi. Pia alieleza kuwa wajibu wa kila mmoja ni kuhakikisha watoto wanakuwa kwenye ustawi bora katika makuzi yao ilikuweza kutimiza malengo yao mbalimbali pindi watakapofika ukubwani.

kwa upande wake, mmoja wa wazee wa Mila wilayani hapa, Rashid Yusufu Sekamba alisema kuwa watahakikisha wanaachana na mila potofu ilikuendana na wakati ikiwemo suala la unyago kwa watoto wa kike.

“Tumesikia sana kilio chenu watoto, juu ya mila potofu hasa unyago, tutachukua hatua na hata kulimaliza..Mimi sijui huko kwenye unyago wanafundisha mambo gani, ila kama  namcheza mtoto bado yupo shule, ni lazima aende akajaribu kwa vitendo hili si sawa. Sasa unadhani hili ni sawa?, si sawa wazee wa mila tutaangalia namna ya kuachana nalo” alisema Sekamba.

Katika maadhimisho hayo, ambayo yaliratibiwa na Halimashahuri ya Bagamoyo kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, Mkuu wa Wilaya alikabidhi baiskeli moja ya walemavu (wheelchair), pamoja na kupokea kandambili pea 300, vyote vilivyoolewa na Asasi ya TRACED. Sherehe za mwaka huu za mtoto wa afrika yenye kauli mbiu, “Kuondoa mila potofu zenye kuleta madhara kwa watoto: Ni jukumu letu sote”.

Kwa upande wao wajumbe mbalimbali waliotoka asasi za kiraia ndani ya wilaya hiyo walipongeza shughuli hiyo. Asasi hizo ni pamoja na HELP Foundation, Mkombozi, TRACED, HakiMtoto Foundation, BAKA, Compassion na wengine wengi.

Kwa upande wa watoto hao waliweza kuelezea na kutoa kero mbalimbali dhidi ya vitendo wanavyofanyiwa na jamii ikiwemo unyanyasaji na ukatili huku wakiomba kutambua watoto ni taifa la leo  hivyo linahitaji kulindwa.
 
Kupitia risala yao, watoto hao mbele ya DC, walitaka kuthaminiwa,ulinzi, kusikilizwa na yale yote ya msingi.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo