MADIWANI RUNGWE WAPITISHA AZIMIO LA KUPEWA HADHI YA KUWA MKOA

Mkuu wa wilaya ya Rungwe Crispin Meela

MADIWANI wa Halmashauri  ya Wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya wamekubali kupendekeza azimio la kuugawa Mkoa wa Mbeya kama walivyoagizwa na Rais Jakaya Kikwete na kukubaliana kuwa Mkoa mpya uitwe Rungwe na makao makuu ya Mkoa yawe Tukuyu.

Pendekezo hilo limetolewa jana katika kikao maalum cha Baraza hilo kilichojadili kuugawa mkoa huo ambapo pendekeza hilo liliwasilishwa na Mkurugenzi wa Halmashauri wa Wilaya ya Rungwe Noel Mahyenga kwa madiwani na kusema kuwa kutokana na agizo la Rais kutaka kuugawa Mkoa wa Mbeya na wao kutaka Mkoa mpya uitwe Rungwe.

Alisema kuwa kikao cha kamati ya fedha uongozi na mipango  kilijadili suala hilo kupitia mapendekezo ya wataalam ambayo yalikidhi vigezo vyote na kuwa kutokana na historia ya Wilaya hiyo ilivyokuwa na Jiografia nzuri katika shughuli za kiuchumi ipo haja ya kupitisha azimio la Wilaya hiyo kuwa Mkoa.

Aliongeza kuwa Wilaya ya Rungwe inavivutio vingi vya utalii vipatavyo 19 miongoni mwa maeneo hayo ni kambi ya uvuvi ya Isongole,daraja la mungu ziwa ngozi na mlima Rungwe na pia kuna uwanja wa ndege (airstrip) ambao unaweza kutumiwa katika shughuli za kiutawala,kibiashara na kitalii zitakazopanuka na kuongeza pato mara dufu.

Kutokana na hali hiyo madiwani walipitisha azimio hilo la Rungwe kuwa Mkoa kwa asilimia 90 na kuzitaja wilaya zitakazounda Mkoa huo kuwa ni Ileje,Kyela,Rungwe na Busokelo ambayo itapandishwa hadhi kuwa Wilaya kamili badala ya Halmashauri kama ilivyo sasa,

Baada  ya kumalizika kwa baraza hilo la madiwani,Mkuu wa Wilaya ya Rungwe Chrispin Meela aliitisha kikao cha Baraza la ushauri (DCC)akiwashirikisha maafisa watendaji wa kata wenyeviti wa vyama vya siasa wakuu wa idara na wananchi wa kawaida kwa lengo la kujadili suala la Mkoa Mpya.

Katika kikao hicho wananchi na viongozi wote wa Serikali na Taasisi binafsi  waliunga mkono suala hilo na kutoa azimio la kutaka Rungwe ipandishwe hadhi ya kuwa Mkoa  kama walivyopendekeza madiwani katika baraza lao.

Waliongeza kuwa Wilaya za Mbarali,Mbozi,Momba,Chunya na Mbeya zibaki kuwa Wilaya huku Mkoa uwe Rungwe na Wilaya zake ziwa Kyela,Ileje Rungwe na Busokelo na makao makuu ya Mkoa yawe Tukuyu ka walivyopendekaza Madiwani katika kikao chao.
 
Na Ibrahim Yassin


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo