BANDA LA MALIASILI NA UTALII SABASABA MSIMU HUU NI NOMA



Wizara ya Maliasili na Utalii inashiriki kwenye maonyesho ya Biashara ya Kimataifa ya SABASABA mwaka huu yanayofanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius.K.Nyerere, Saba Saba, Barabara ya Kilwa.

Wizara inawakaribisha wananchi wote wenye kiu ya kuona na kuelimika kuhusu shughuli za Utalii, Ufugaji Nyuki, Uhifadhi wa Misitu, Malikale na Wanyamapori. Ikumbukwe kuwa Banda la Maonesho la Wizara miaka yote huwavutia watu wengi wanaoshiriki katika maonesho ya Viwanda na Biashara  hali ilinayowapelekea watu wengi kushindwa kuingia ndani kuona wanyama kutokana na umati mkubwa wa watu wanaofurika hasa inapokaribia kilele cha maonyesho.

Wizara inapenda kuwajulisha wananchi wanaopenda kujielimisha na kuona shughuli mbalimbali za Wizara kutembelea banda kuanzia Mwanza wa maonyesho badala ya kusubiri siku ya ufunguzi Julai 4 mwaka huu ambapo watu hufulika kiasi cha wengi kushindwa kutii kiu zao wafikapo bandani.
Aidha, katika kuimalisha utalii wa ndani Wizara imeandaa safari za kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Mikumi kwa gharama nafuu ambapo  mtu mzima atalazimika kulipa Tsh 15,000/-  na mtoto Tsh 5,000/- ikiwa ni gharama za usafiri kutoka viwanya vya Sabasaba hadi hifadhini na kurejea siku hiyo hiyo jijini Dar es Salaam.
Sambamba na hilo Wizara imetoa ufadhili kwa vikundi vya asali kutoka wilaya zote nchini zenye wafugaji nyuki ili kutoa fursa kwa wananchi kujifunza juu ya umuhimu wa asali mwilini. Vikundi hivi vinapatikana katika Banda la Asali litakalokuwa na maonyesho ya asali na bidhaa zitokanazo na nyuki.
Wizara haijawasahau wananchi wanaopenda kutunza mazingira kwa kupanda miti ya matunda, kivuli pamoja na mapambo kwa kuhakikisha inawaletea miche mbalimbali bandani inayouzwa kwa bei nafuu.
Ndani ya banda wananchi watapata fursa ya kukutana na wadau mbalimbali wa sekta ya utalii, wanyamapori na mambo ya kale watakaokuwa wanatoa elimu juu ya jambo lolote litakalokuwa linamtatiza mwananchi aliyefika bandani hapo.
Miongoni mwa wanyamapori hai watakaokuwepo ni kama vile Chui, Nyoka, Ndege wa aina mbalimbali pamoja na mfalme wa pori SIMBA.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo