MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM AZUNGUMZIA WALIVYOJIPANGA KUMPOKEA OBAMA KESHO

 
 
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, SAID MECK SADICK, amesema serikali imechukua tahadhari zote katika kuhakikisha shughuli zote za wananchi za kibiashara zinaendelea kama kawaida wakati wa ziara ya rais wa Marekani Barack Obama.
 
Aidha mkuu huyo wa mkoa amesema katika kipindi hicho wafanyabiashara kutoka mikoani na ndani ya jiji wataendelea kuingiza bidhaa zao katika masoko kama kawaida bila kuzuiliwa, na kwamba si barabara zote zitakazofungwa na kutolea mfano wa barabara itakayofungwa kuwa ni barabara ya Nyerere ambayo wageni wengi hutumia na kwamba ziara hiyo haitaathiri maonesho ya 37 biashara maarufu kama sabasaba yanayoendelea katika viwanja vya Mwl. JULIUS NYERERE.

Rais wa Marekani Barack Obama anatarajia kuzuru Tanzania siku ya jumatatu ambapo miongoni mwa masuala atakayoangazia ni pamoja na kuhamasisha demokrasia na kukuza fursa za kiuchumi.

Maandalizi ya mapokezi ya Rais Obama yamezidi kupamba moto hasa katika jiji la Dar-es salaam ambapo ndipo kituo chake cha kwanza kwa rais huyo nchini Tanzania huku suala la usafi na matengenezo katika barabara nyingi Jijini likionekana kupewa kipaumbele tofauti na siku zote.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo