HALMASHAURI YA MAKETE YAPONGEZWA KWA KUSAMBAZA VIFUSI VILIVYOKAA MUDA MREFU


Wananchi wa kata ya Iwawa wilayani Makete ambao wanazitumia barabara za mitaa zilizokuwa zimelundikwa vifusi kwa muda mrefu, wameipongeza halmashauri yao kwa kusikia kilio chao na kuanza kusambaza vifusi hivyo hali iliyopelekea barabara hizo kupitika kirahisi

Hatua hiyo imeokelewa kwa furaha na wakazi hao huku wengine wakiitaka halmashauri hiyo wakati mwingine kuweka vifusi kwa kulingana na hali ya hewa ili kuondoa usumbufu wa vifusi hivyo kukaa muda mrefu

Mtandao huu umeshuhudia zoezi la usambazaji vifusi kwenye barabara hizo likiwa limekamilika na magari yakipita kwani awali barabara hizo zilifungwa kutokana na matengenezo

Jumatatu ya wiki hii mhandisi wa ujenzi wilaya ya Makete Eng. Samweli Ndoveni alinukuliwa akisema usambazaji huo wa vifusi utaanza Jumanne ya wiki hii, ambapo mtandao huu umeshuhudia zoezi hilo likitekelezeka kama alivyosema


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo