MAHAKAMA YAMWACHIA HURU DIWANI WA KATA YA MIVINJENI FRANK NYALUSI

Mahakama ya hakimu mkazi manispaa ya Iringa imemuachia huru diwani wa kata ya mivinjeni FRANK NYALUSI na wenzake watatu JOSEPH MGIMWA,WILLIUM MGUNDA NA TIMOTHEO MSENJA  waliokuwa wanashikiliwa na jeshi la polisi kwa makosa matatu.
 
Akiwasomea mashtaka yao katika mahakama ya hakimu mkazi mshtakiwa wa pili na watatu FRANK NYALUSI na JOSEPH MGIMWA wanashtakiwa kwa kosa la kuwashawishi watu kufanya fujo na kuandamana bila kibali hivyo kusababisha uvunjwaji wa amani katika barabara ya mashine tatu tarehe 19 mwezi huu.
 
Wakati huo huo mahakama imewashtaki watuhumiwa wote (4) kwa kosa la pili la kuandamana na kufanya mkutano bila kibali cha kamanda mkuu wa jehi la polisi hivyo kusababisha vurugu katika eneo la mashine tatu,na kosa la tatu mahakama ime washtaki watuhumiwa na 2 na namba tatu kwa kosa la kushawishi watu kufanya fujo na kufanya uhalibifu wa mali likiwemo gari la kikosi cha zima moto mkoani hapa.
 
Washitakiwa wote wameachiwa huru kwa dhamana ya shilingi milioni 1  huku mahakama ikiwataka washitakiwa wa nne kuto jihusisha na sehemu yoyote yenye dalili ya uvunjwaji wa amani.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo