ALIYENUSURIKA AJALI GHOROFA LILILOPOROMOKA DAR ASIMULIA MKASA MZIMA

Rais Jakaya Kikwete na mkewe, Salma wakimjulia hali Mohammed Ally Bhamji, mmoja wa majeruhi wa ajali ya jengo lililoporomoka Ijumaa iliyopita Barabara ya Morogoro na Indira Ghandhi, Dar es Salaam, walipomtembelea Kitengo cha Mifupa cha Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MOI) jana. (Picha na Ikulu).
Mmoja wa majeruhi  katika jengo la ghorofa 16 lililodondoka katika Mtaa wa Indira Ghandhi juzi jijini Dar es Salaam,  ameelezea jinsi alivyonusurika kifo katika ajali hiyo akiwa ghorofa ya 15.

Selemani Said (26) ambaye ni miongoni mwa majeruhi wanne waliolazwa katika Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI) anasema wakati akiwa gorofa ya 15 alishuhudia jengo lilivyokuwa likianza kushuka. 
 
Majeruhi huyo ambaye ni fundi ujenzi, alisema wakati ajali hiyo ikitokea asubuhi, alishuka na jengo hilo hadi chini na baada ya hapo, alipoteza fahamu na kushtukia akiwa hospitali.
 
“Siku ile ilikuwa ni siku ya kumwaga zege. Tulikuwa wengi wakiwemo vibarua ambao jengo linapofikia hatua ya kumwaga zege, huwa linahitaji vibarua wengi, nikiwa najiandaa kuanza ujenzi, mara nilihisi kama jengo linaanguka, nilipoangalia nje niliona ninashuka nalo,” alisema Said.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo