
---
Dar es Salaam.
Idadi
ya watu waliokufa kutokana na kufukiwa na kifusi cha jengo la ghorofa
16 lililoporomoka juzi asubuhi jijini Dar es Salaam, imefikia 22.
Habari
zilizopatikana kutoka eneo la uokoaji na kuthibitishwa na Kamanda wa
Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova zinaeleza kuwa
miili iliyopatikana imepelekwa Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Jengo
hilo lililokuwa likijengwa mkabala na Msikiti wa Shia Ithnasheri ulioko
Barabara ya Indira Gandhi na Kampuni ya Lucky Construction Limited
liliporomoka saa 2.30 asubuhi wakati mafundi na vibarua wakiendelea na
ujenzi huku chini watoto wakicheza mpira na mama lishe wakiendelea na
biashara zao kama kawaida.
Rais Kikwete
Rais Jakaya Kikwete ambaye jana pia alifika katika eneo la tukio, kama ilivyokuwa juzi, alipata taarifa fupi ya maendeleo ya uokoaji kutoka kwa Mkuu wa Mkoa, Said Meck Sadik na Kamanda Kova.
Rais Jakaya Kikwete ambaye jana pia alifika katika eneo la tukio, kama ilivyokuwa juzi, alipata taarifa fupi ya maendeleo ya uokoaji kutoka kwa Mkuu wa Mkoa, Said Meck Sadik na Kamanda Kova.
Baada
ya kupewa taarifa hiyo, Rais Kikwete alimwagiza Kamanda Kova
kuhakikisha wahusika wanakamatwa akiwamo Mkadiriaji Majengo (Quantity
surveyor), mchora ramani za majengo (Architecturer), Mhandisi Mshauri
(Consultant) na Mhandisi wa Jiji la Dar es Salaam.
Juzi baada ya kutembelea eneo la tukio, Rais Kikwete aliagiza wahusika wote wa ujenzi huo wachukuliwe hatua kali.
Habari
zilizopatikana jana zilidai kuwa Diwani wa Kata ya Goba, Wilaya
Kinondoni, Ibrahim Kisoka ambaye ndiye mmiliki wa kampuni ya ujenzi, na
Mhandisi Mshauri kwa pamoja wamejisalimisha Kituo Kikuu cha Polisi na
hadi saa 8:00 jana mchana walikuwa wakihojiwa.
Awali
Kamanda Kova aliwaambia waandishi wa habari kuwa amemtaka mmiliki wa
Kampuni ya Lucky Construction Limited ambaye ni Diwani wa Kata ya Goba,
Kisoka na wahusika wengine kujisamilisha kituo cha polisi, kabla
hawajaamua kutumia nguvu kumtafuta.
Pinda atembelea eneo la tukio
Waziri Mkuu Mizengo Pinda alifika eneo hilo saa 3:41 asubuhi, kujionea hali ilivyo, lakini hakutoa tamko lolote. “Sina la kusema,” alisema Waziri Mkuu alipoulizwa na waandishi wa habari kutoa kauli ya serikali kuhusiana na tukio hilo.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda alifika eneo hilo saa 3:41 asubuhi, kujionea hali ilivyo, lakini hakutoa tamko lolote. “Sina la kusema,” alisema Waziri Mkuu alipoulizwa na waandishi wa habari kutoa kauli ya serikali kuhusiana na tukio hilo.
Hata
hivyo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge,
William Lukuvi aliyefuatana na Pinda, alisikika akimwagiza Kamanda Kova
kuhakikisha mchora ramani wa jengo hilo naye anatiwa nguvuni kwa kuwa
jengo hilo lilikuwa la ghorofa 10, lakini likajengwa hadi 16. Mtu
mwingine ambaye anatafutwa na jeshi la polisi kukamatwa ni Mhandisi
Mshauri.
Lukuvi
alimwagiza Kova kuwa watu waliokuwa karibu na jengo jingine la ghorofa
15 lililojengwa na mkandarasi huyo, kuhama mara moja na ubomoaji
ufanyike bila kuleta madhara.