BEI YA MKAA WILAYANI MAKETE YAZIDI KUPAA


Mkaa huu unauzwa sh. 8000/= kutoka 5000/= ya awali
Bei ya mkaa wilayani Makete inazidi kupanda siku hadi siku kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha wilayani humo

Kupanda mara kwa mara kwa bei hizo kumesababishwa na mvua zinazoendelea kunyesha wilayani humo hivyo kupelekea ugumu wa kutengeneza mkaa hivyo wengi wa waandaaji wa mkaa kuacha

Mmoja wa muuzaji mkaa aliyejitambulisha kwa jina la Tweve amesema idadi ya waliokuwa wakiandaa mkaa kutoka kwenye kijiji chake cha Ivalalila wameacha kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha wilayani humo

“Unajua uchomaji wa mkaa unakuwa mgumu sana kipindi hiki, ukianda magogo kwa ajili ya kuyachoma ili upatikane mkaa, mvua inayesha na moto unazima, kwa hiyo sisi tunaojitahidi hivyo hivyo inatulazimu kupandisha bei” alisema Tweve

Bei ya gunia la mkaa hivi sasa imepanda kutoka sh. 8000/= ambapo hivi sasa gunia linauzwa kati ya shilingi 10,000 hadi 15,000/= jambo linalowapa tabu watumiaji wa mkaa huo

Hata hivyo kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha wilayani Makete zinapelekea wananchi wengi kutumia zaidi mkaa kuliko kuni kutokana na kuni hizo kulowa, lakini bidhaa hiyo ya mkaa nayo inazidi kupungua kutokana na wauzaji kuwa wachache


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo