Na Immaculata Makilika na Lorietha Laurence Maelezo
CHAMA cha wasioona Tanzania
idara ya wanawake kimetoa wito kwa wanajamii na wadau mbalimbali
kushirikisha wasioona katika mchakato wa uundwaji wa Katiba mpya
nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari
leo jijini Dar es salaam Mweyekiti wa Chama cha Wasioona Idara ya
Wanawake amesema kuwa wanawake wakishirikishwa katika uundwaji wa
katiba mpya watakuwa na sauti moja katika kudai maslahi yao.
Ameeleza kuwa lengo kuu ni
kuwawezesha wanawake kuwa na sauti moja katika kudai maslahi yao hasa
masuala muhimu yanayowahusu wasioona kama jamii yenye mahitaji sawa na
wengine.
“Wanawake wasioona wakipewa nafasi
katika katiba mpya wataweza kutambuliwa na kuthaminiwa katika masuala
yote ya kijamii kama vile, siasa, elimu,uchumi na Utamaduni.”Alisema Bi.
Kulangwa.
Wakati huohuo Katibu wa chama
hicho Bi. Doroth Kaihuzi amehamasisha jamii ichangie katika harakati za
maendeleo kwa wasioona katika nyanja mbalimbali ikiwemo uhamasishaji
juu ya mchakato wa uundwaji wa katiba mpya.