WATUMISHI WA HALMASHAURI YA SIMANJIRO WAKABWA KOO NA MADIWANI

BARAZA la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara limeagiza watumishi wa halmashauri hiyo kufuatilia  mchakato wa ujenzi wa eneo huru la biashara (EPZ) Mirerani kwani ni ahadi ya Rais Jakaya Kikwete.
 
Aidha madiwani hao walisema  kuwa wakati wa kampeni ya uchaguzi wa mwaka 2010 Rais Jakaya Kikwete na Makamu wa Rais Dk Gharib Bilal,kwa nyakati tofauti wilayani humo walitoa ahadi ya ujenzi wa EPZ kwenye mji mdogo wa Mirerani.
 
Waliongeza kuwa  eneo linalopaswa kujengwa EPZ lilishatengwa kwa muda mrefu,hivyo mchakato wa ujenzi wake ulitakiwa kuanza tangu hapo awali,lakini hadi hivi sasa hakuna hatua zozote zilizofanyika ikiwemo upimaji na michoro ya ujenzi. 
 
Naye Diwani wa kata ya Mirerani Justin Nyari aliongeza kuwa  amefuatilia suala hilo muda mrefu kwenye Wizara ya Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi ili kubaini hatma ya mradi huo na anajibiwa kuwa wanasubiri taarifa ya halmashauri.
 
 Alisema kuwa Halmashauri inatakiwa ifuatilie hili suala kwani nimekuwa nikipiga simu wanadai kuwa wanatusubiri majibu ya halmashauri juu ya matumizi bora ya aridhi,wenzetu wa Kia wapo kwenye mchakato wa upimaji.  
 
Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya hiyo,Peter Tendee alisistiza kuwa  hivi karibuni kwenye kikao cha ushauri cha mkoa huo (RCC) alizungumzia kuhusiana na EPZ ya Mirerani na akaelezwa kuwa viongozi hao watalishughulikia.
 
 “Kwa kweli  suala hili tulishalifikisha mkoani wakatujibu kuwa ngazi za juu wanashughulikia,tunapaswa kusubiri utekelezaji wake kwani mradi huu umechukua muda mrefu na hadi sasa ujenzi wake haujaanza,” alisema Tendee.
 
 Kwa upande wake Diwani wa kata ya Naberera,Sumleck Ole Sendeka alisema utekelezaji wa ujenzi wa EPZ ya Mirerani,ulitakiwa kuanza ili kuinufaisha wilaya hiyo kupitia mradi huo lakini hadi hivi sasa mchakato wake umechukua muda mrefu kutekelezwa.  
 
 Alibainisha kuwa EPZ imekuwa hadithi ndefu kwani madiwani wa kipindi cha mwaka 2005/2010 walikwenda Dar es salaam kuona pamoja na kujifunza kupitia EPZ ya Ubungo ili iwe somo kwao sasa mbona ahadi ya Rais haitimizwi.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo