WANAFUNZI 3090 wa Wilaya ya Hanang’ katika Mkoa wa
Manyara wa shule za msingi waliofaulu na kuchaguliwa kujiunga na kidato cha
kwanza kwenye shule za sekondari kwa mwaka 2013 wameanza rasmi masomo yao.
Taarifa
hiyo imetolewa na Mkuu wa wilaya ya Hanang’ Christina Mndeme wakati
akiongea kwenye kikao cha wadau wa elimu wa wilaya hiyo kuhusiana na
changamoto mbalimbali zinazowakabili wilayani humo.
Alisisitiza kuwa wanafunzi hao waliofaulu
wameanza masomo yao kwani wilaya yao haina tatizo la ukosefu wa vyumba vya
madarasa ya shule za sekondari ambazo wanafunzi hao waliofaulu wamepangiwa.
Alisema
kuwa mwaka 2012 wilaya yao ilishika nafasi ya nne kwa ufaulu kwenye mkoa
huo na mwaka 2011 ilishika nafasi ya tatu hivyo mwaka huu wa 2013 wamejipanga
washike nafasi ya kwanza kwenye mkoa huo na ngazi ya kanda.
Mkuu wawilayahiyo amewaasa walimu wa wilaya hiyo
kuzifikisha changamoto walizonazo kwa muajiri wao Mkurugenzi Mtendaji wa
halmashauri hiyo Felix au yeye mkuu wa wilaya hiyo,kuliko kuzipelekwa kwa
viongozi wa chama cha walimu (CWT).
“Inashangaza
kuwa matatizo yenu mnakuwa mnayafikisha sehemu ambayo siyo husika hivyo
mnashindwa kupatiwa msaada mfano mwezi uliopita tulilipa madeni ya walimu 38 na
mwezi huu tumelipa madeni 47.Alishangaa mkuu wa wilaya hiyo.
Aidha alisema kuwa kutokana na kauli mbiu yake
ya elimu,kazi na nidhamu zitaondoa umaskini Hanang’ anatarajia walimu,wanafunzi
na wadau wote wa elimu wa wilaya hiyo watapandisha kiwango cha ufaulu kwa mwaka
huu.
“Tunatakiwa
tushirikiane kwa pamoja mimi na ninyi wadau wa elimu na ninyi walimu muache
kushiriki migomo isiyokuwa na tija tufanyeni kazi kwa bidii kama kuna tatizo
tukae mezani tulijadili na hatimaye tulimalize,” alisema Mndeme.