WACHEZAJI WA NIGERIA WAAHIDIWA NGONO WIKI NZIMA ENDAPO WAKICHUKUA USHINDI

Prostitutes

Machangudoa nchini Nigeria wamesema wamefurahia sana ushindi wa Super Eagles dhidi ya Ethiopia katika mashindano ya AFCON yanayoendelea nchini Afrika ya Kusini.
Machangudoa hao kupitia chama chao cha aegis of Nigeria Association of Prostitutes  wamewasisitiza wachezaji wa timu ya taifa ya Nigeria kujitahidi na kushinda kombe hilo. Katika taarifa iliyotolewa na kusainiwa na katibu mkuu wa chama hicho Jessica Elvis. 
 “Tunapenda kuwapongeza wachezaji na makocha wa timu ya taifa ya Nigeria, Super Eagles kwa kufuzu kuingia robo fainali raundi inayofuatia ya mashindano. Tungependa kuwapa uhakika wa sapoti yetu ili waweze kuleta ushindi nyumbani. 
"Katika kuonyesha sapoti yetu kwa timu ya taifa, tutatoa ofa ya wiki moja ya mapenzi bure kwa Super Eagles ikiwa watashinda ubingwa wa Afrika," alisema katibu mkuu wa chama hicho cha machagundoa.
Inasemekana baadhi ya wanachama wa chama hicho wapo nchini South Africa wakiisapoti timu hiyo kwenye mashindano ya AFCON.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo