
Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar,Balozi Self Ali
Idd,akimkabidhi Mkuu wa Vodacom Tanzania,Kanda ya kaskazini,Bw.Philemon
Chacha tuzo ya mchangiaji bora wa michango ya wanachama katika mfuko
wa pensheni wa NSSF kwa makampuni ya mawasiliano nchini.Vodacom imeshinda
tuzo hiyo na kukabidhiwa wakati wa hafla ya ufunguzi wa mkutano wa tatu
wa wadau wa mfuko wa NSSF uliofanyika Mount Meru Hoteli jijini Arusha.

Mkuu wa Vodacom Tanzania,Kanda ya kaskazini,Bw.Philemon Chacha akionesha
tuzo ya mchangiaji bora wa michango ya wanachama katika mfuko wa pensheni
wa NSSF kwa makampuni ya mawasiliano nchini.Tuzo hiyo ilitolewa jana
katika mkutano wa tatu wa wadau wa NSSF na Makamu wa pili wa Rais wa
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Balozi Self Ali Idd.

Mkuu wa Vodacom Tanzania,Kanda ya kaskazini Bw.Philemon Chacha akiwa
na Meneja wa uendelezaji biashara wa kanda hiyo Bw. Philemon Matoi na
tuzo waliyokabidhiwa kwa niaba ya kampuni ya vodacom Tanzania baada
ya kuongoza kwa makampuni yote ya mawasiliano katika uchangiaji wafanyakazi
wake katika mfuko wa pensheni ya NSSF, tuzo hiyo ilitolewa na makamu
wa pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Balozi Self ali Idd
katika mkutano wa tatu wa wadau wa mfuko huo, Mount Meru hoteli jijini
Arusha.

picha ya pamoja ya washindi wa tuzo za wachangiaji bora wa mfuko
wa hifadhi ya jamii ya NSSF pamoja na Makamu wa pili wa Rais wa Serikali
ya mapinduzi Zanzibar Balozi, Self Alli Idd pamoja na viongozi wengeni
wa mfuko wa NSSF.
--
Kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania imeshinda tuzo ya kampuni
bora ya mawasiliano nchini inayowasilisha vema michango ya wafanyakazi
wake katika Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii - NSSF.
Tuzo hiyo imekabidhiwa kwa Vodacom jana na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd katika hafla ya ufunguzi wa mkutano wa tatu wa wadau wa NSSF unaofanyika jijini Arusha
Akizungumzia tuzo hiyo Ofisa Mkuu wa Rasilimali Watu wa Vodacom Dk. Fred Mwita amesema tuzo hiyo ni matokeo ya Vodacom kujali masilahi ya wafanyakazi wake ikiwemo suala la mafao.
"Pamoja na kwamba tunatekeleza wajibu huo kwa mujibu wa sheria lakini ushindi huu ni kielelezo cha udhati na umakini wetu katika kutimiza kila wajibu unaotuhusu kwa wafanyakazi wetu."Amesema Dk Mwita
Amesema Vodacom yenye wafanyakazi zaidi ya 500 imekuwa ikiweka kipaumbele cha upekee katika masilahi na masuala yanayowahusu wafanyakazi kwa kile inachoamini kuwa mafanikio ya kampuni yapo mikononi mwa wafanyakazi hao katika kujibidiisha katika majukumu yao.
Ameutaja ushindi huo kuwa ni ufahari kwa Vodacom kwani inatambua kuwa umepitia mchakato uliokuwa na vigezo vigumu vya ushindani na kwamba inaijengea Vodacom heshima na taswira chanya miongoni mwa jamii ndani na nje ya nchi.
"Vodacom imekuwa mwajiri mzuri ikivutia vijana na wanataaluma mbalimbali na kwamba kwetu sisi tuzo hii itazidi kudhihirisha hilo na kuwafanya wafanyakazi wetu kufanya kazi kwa kujiamini bila hofu juu ya mafao yao."
Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi za Jamii (NSSF), Crescentius Magori, akizungumza katika ufunguzi wa mkutano huo alisema kampuni ya Vodacom,wafanyakazi wake asilimia 95 wamekuwa wakilipiwa vyema makato yao.
"kampuni hii tunaikabidhi tuzo hii kutokana na umahiri wake katika kuwasilisha vyema michango ya wafanyakazi wake pamoja na wafanyakazi wake wote kuendelea kuwa wanachama wa NSSF licha ya baadhi kuhamishwa vitengo"alisema Magori.
Tuzo hiyo, ilipokelewa na Mkuu wa Vodacom Kanda ya Kaskazini, Philemon Chacha kutoka kwa Balozi Idd ambaye pia alipongeza kampuni hiyo ya Vodacom kwa utendaji mzuri na kuwa wachangiaji wazuri wa NSSF.
Makamu huyo wa Rais wa Zanzibar pia alitoa wito kwa waajiri nchini, kuwasilisha katika mifuko ya jamii makato ya wafanyakazi wao kwa wakati kwani kutowasilisha ni kosa la jinai.
Tuzo hiyo imekabidhiwa kwa Vodacom jana na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd katika hafla ya ufunguzi wa mkutano wa tatu wa wadau wa NSSF unaofanyika jijini Arusha
Akizungumzia tuzo hiyo Ofisa Mkuu wa Rasilimali Watu wa Vodacom Dk. Fred Mwita amesema tuzo hiyo ni matokeo ya Vodacom kujali masilahi ya wafanyakazi wake ikiwemo suala la mafao.
"Pamoja na kwamba tunatekeleza wajibu huo kwa mujibu wa sheria lakini ushindi huu ni kielelezo cha udhati na umakini wetu katika kutimiza kila wajibu unaotuhusu kwa wafanyakazi wetu."Amesema Dk Mwita
Amesema Vodacom yenye wafanyakazi zaidi ya 500 imekuwa ikiweka kipaumbele cha upekee katika masilahi na masuala yanayowahusu wafanyakazi kwa kile inachoamini kuwa mafanikio ya kampuni yapo mikononi mwa wafanyakazi hao katika kujibidiisha katika majukumu yao.
Ameutaja ushindi huo kuwa ni ufahari kwa Vodacom kwani inatambua kuwa umepitia mchakato uliokuwa na vigezo vigumu vya ushindani na kwamba inaijengea Vodacom heshima na taswira chanya miongoni mwa jamii ndani na nje ya nchi.
"Vodacom imekuwa mwajiri mzuri ikivutia vijana na wanataaluma mbalimbali na kwamba kwetu sisi tuzo hii itazidi kudhihirisha hilo na kuwafanya wafanyakazi wetu kufanya kazi kwa kujiamini bila hofu juu ya mafao yao."
Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi za Jamii (NSSF), Crescentius Magori, akizungumza katika ufunguzi wa mkutano huo alisema kampuni ya Vodacom,wafanyakazi wake asilimia 95 wamekuwa wakilipiwa vyema makato yao.
"kampuni hii tunaikabidhi tuzo hii kutokana na umahiri wake katika kuwasilisha vyema michango ya wafanyakazi wake pamoja na wafanyakazi wake wote kuendelea kuwa wanachama wa NSSF licha ya baadhi kuhamishwa vitengo"alisema Magori.
Tuzo hiyo, ilipokelewa na Mkuu wa Vodacom Kanda ya Kaskazini, Philemon Chacha kutoka kwa Balozi Idd ambaye pia alipongeza kampuni hiyo ya Vodacom kwa utendaji mzuri na kuwa wachangiaji wazuri wa NSSF.
Makamu huyo wa Rais wa Zanzibar pia alitoa wito kwa waajiri nchini, kuwasilisha katika mifuko ya jamii makato ya wafanyakazi wao kwa wakati kwani kutowasilisha ni kosa la jinai.