TUME YA MABADILIKO YA KATIBA YAKUTANA NA WAWAKILISHI WA MAKUNDI YA WATU WENYE ULEMAVU

 Mwenyekiti wa kamati ya uwasilishaji wa mapendekezo ya muundo wa mabaraza ya Katiba kwa jamii ya watu wenye ulemavu, Bw. David Nyendo (kushoto) akiwasilisha maoni yake ya kamati hiyo kwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba katika mkutano baina yao uliofanyika leo (jumatano Feb. 13, 2013) katika ofisi za makao makuu ya Tume Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mjumbe wa Tume, Dkt. Salim Ahmed Salim.
 Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba (kulia) akizungumza na wawakilishi wa makundi ya jamii ya watu wenye ulemavu ukiongozwa na Mwenyekiti wa kamati hiyo, Bw. David Nyendo (kushoto) mara baada ya kufika katika makao makuu ya Tume leo (jumatano Feb. 13, 2013) kuwasilisha mapendekezo yao juu ya muundo wa mabaraza ya Katiba kwa jamii ya watu wenye ulemavu. Wa pili kushoto ni Mjumbe wa Tume, Dkt. Salim Ahmed Salim.
Mkalimani wa lugha za alama kwa watu wenye ulemavu wa kusikia kutoka Umoja wa Miradi ya Viziwi Tanzania (UMVITA), Bi. Ruth Hope akisaidia uelewa wa lugha ya mawasiliano kwa watu wa jamii ya walemavu wa kusikia katika mkutano baina yao na Tume ya Mabadiliko ya Katiba. Walemavu hao waliunda kamati iliyokutana na Tume ili kuwasilisha mapendekezo yao juu ya  muundo wa mabaraza ya Katiba kwa jamii yao.Picha Zote na Tume ya Katiba


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo