SERIKALI KUU YATAKIWA KUZIHESHIMU HALMASHAURI


 
Na Ibrahim Yassin,Kyela

MWENYEKITI wa baraza la madiwani katika halmashauri ya wilaya Kyela ,Gagriel Kipija aliesema kuwa ipo haja sasa kwa serikali kuu kwa kuziheshimu hamashauri hapa nchini kuliko ilivyo sasa

Alisema kuwa halmashauri nyingi hazitendewi haki na serikali kwa mambo mengi kiasi cha kukwamisha shughuli za maendeleo na kuwapa wakati mgumu madiwani kujieleza pale wanapohojiwa na wananchi wao pale wanapoona miradi mingi inasinzia

Kauli hiyo ameitoa jana kwenye kikao cha dharura cha baraza la madiwani ambao waliagizwa na serikali kuu kupitisha bajeti haraka kabla ya kikao cha bunge kuanza  na kupitisha bajeti ya Tshs,23,437,095,997,00  kutoka katika vyanzo mbalimbali vya mapato

Mwenyekiti huyo wa halmashauri alisema kuwa wamekuwa wakipanga bajeti zao kwa kutegemeana na ruzuku kutoka serikali kuu cha ajabu fedha za serikali kuu zimekuwa hazifiki katika hamashauri na kama zikifika hazifiki kwa wakati kiasi cha kukwamisha shughuli za maendeleo

Alisema kitendo hicho cha serikali kushindwa kupeleka fedha katika halmashauri ni kitendo cha dharau ambacho serikali inabidi kujisahisha na hari ikiendelea hivyo wao hawataendelea kupitisha bajeti ambazo mwisho wake jamii itawaona kuwa ni waongo kwa baadhi ya miradi kushindwa kutekelezeka kwa  wakati au kushindwa kutekelezeka kabisa baada ya
kukosekana kwa fedha ambazo serikali kuu haizipeleki kwenye halmashauri

Katika baraza hilo pia madiwani hao walitaka bajeti hii ya 2013/14 iweze kushughulikia baadhi ya kero nyingi ambazo zimedumu kwa muda mrefu bila ya kuzishughulikia

Diwani wa kata ya Busale Ezekiel Msyani alisema kuwa moja ya kero kubwa na ambayo imedumu kwa muda mrefu ni tatizo la maji na kuiomba serikali katika bajeti hii mpya kuhakikisha kuwa wanaiangalia kwa umakini kero ya maji na kulazimika kutumia baadhi ya fedha katika mapato ya ndani kuyalazimisha kwenda kushughulikia tatizo hilo la maji

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya Abdallah Mfaume kwa upande wake  alisema kuwa tatizo la halmashauri kutopata fedha kutoka serikali kuu ni la kitaifa na kuwa hivi sasa fedha zitakuja na miradi yote itatekelezeka vizuri

Mkuu wa wilaya Kyela Magreth Malenga alisema kuwa hari hiyo ya serikali kutoleta fedha kwa wakati ni moja ya mambo yaliyofanya halmashauri kushindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo

Na aliwaomba madiwani hao kuwa wavumilivu kwa serikali iliyopo madarakani kwani hivi sasa serikali ina fedha za kutosha za  kuweza kutatua kero mbalimbali zilizopo katika kata zao


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo