OFISI YA CCM YAKOSA HUDUMA YA CHOO KWA MIAKA 15


Na Ibrahim Yassin, Kyela

WANACHAMA wa chama cha Mapinduzi (CCM)wilayani Kyela mkoani Mbeya wapo hatarini kupata magonjwa ya milipuko kutokana na kukosa huduma ya choo kwa muda wa zaidi ya miaka 15 katika ofisi ya chama wilaya,ali inayo walazimu baadhi ya wanachama  kujisaidia katika vyoo vilivyopo kwenye nyumba za jirani na ofisi hiyo.

Kukosekana kwa huduma hiyo ya choo kwa muda mrefu kuna shusha hadhi ya chama hicho kutokana na ukubwa wake na kimekuwa kikipata haibu kubwa hasa pale wanapofika wageni kutoka mikoani ambao wanafika ofisini hapo kwa shughuri za kichama wanapelekwa kujisaidia katika vyoo vilivyopo jirani na ofisa hiyo pindi wanapo hitaji huduma ya choo.

Akitoa majibu kwa waandishi wa habari kuhusu tatizo hilo Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi  walayani Kyela Dkt Hanta Mwakifuna,mbali na kukiri kuwepo na tatizo hilo alisema kuwa yeye kama mwenyekiti amechukua jukumu hilo la kuanza mchakato wa ujenzi  ili kuodoa kero inayoipa kashfa ofisi yake.

Alisema kuwa ofisi yake imetenga kiasi cha tsh,7000,000/ = kwa ajili ya kuanza kuondoa tatizo hili kwa kuweka mipango ya muda mfupi na kwamba wameunda kamati ndogo ya ujenzi yenye wajumbe 6 wakiongozwa na wajumbe 2 wa kamati ya siasa ambapo  kazi hiyo ya ujenzi itakamilika ndani ya siku 90.

Dkt ,Mwakifuna ambaye pia ni diwani wa kata ya Ipinda aliwataja viongozi wengine waliopo kwenye mchakato huo kuwa ni mkuu wa wilaya Magreti malenga (Mwenyekiti)Mwenyekiti wa haimashauri Gabriel  Kipija( makamu)na Patrick Mwampeta (mtunza hazina)ambapo wamekubaliana kila diwani atoe Tsh,90,000 na kila mjumbe wa kamati ya siasa  ya wilaya atatoa Tsh,30,000/-ambao kwa idadi yao watafikisha kiasi hicho cha 7000,000/kitakacho kamilisha ujenzi huo ndani ya siku 90.

Sambamba  na hilo mwandishi wa habari hizi alihoji kuhusu ujenzi wa ofisi ya chama kwamtindo wa ghorofa ulioahidiwa kujengwa na mbunge wa jimbo la Kyela wakati akiomba ridhaa  ya kuwa mbunge kwa wanachama,na wanachama hao walimpa nafasi ya kuwa mbunge lakini amemaliza miaka 8 tangu awe mbunge na hakuna dalili ya kuwepo na ujenzi huo,na kibaya zaidi hata choo tu hakuna.

Akijibu hoja hiyo mwenyekiti mwakifuna,alidai kuwa ni kweli mbunge aliahidi lakini ujenzi huo wa ofisi ya chama kwa mtindo wa ghorofa haujaanza ,na kuwa yeye alipochaguliwa kuwa mwenyekiti  alimkumbusha mbunge juu ya kuanza kwa ujenzi huo ambapo mbunge alimuahidi kuwa ujenzi huo utaanza muda si mrefu .

“Nilipochaguliwa mwenyekiti  wa chama wilaya nilimkumbusha mbunge juu ya ujenzi wa ofisi hiyo kwa mtindo wa ghorofa na mbunge amelipokea na tayali amenipa ramani kilichobakia ni michakato midogo midogo ikikamilika ujenzi huo utaanza”,alisema Dkt Mwakifuna.

Dkt Mwakifuna alimaliza kwa kuwataka wanachama  wa chama cha mapinduzi kuwa na mshikamano na uvumilivu katika kukijenga chama hasa kipindi hiki wanapoelekea kwenye uchaguzi wa wenyeviti wa vijiji na vitongoji ili wananchi wawe na imani na chama hicho na kuendelea kukipa ridhaa ya kuendelea kuongoza nchi.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo