
Mwenyekiti Chama cha Wananchi (CUF),Profesa Ibrahim Lipumba.
---
CHAMA cha Wananchi (CUF), kimemnadi Mwenyekiti wa chama hicho,
Profesa Ibrahim Lipumba kugombea kwa mara nyingine kiti cha urais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2015,
huku yeye binafsi akitangaza neema kwa Watanzania ya kuwajaza fedha
mifukoni.
Katika mkutano wa uzinduzi wa operesheni ya
mchakamchaka kuelekea mwaka 2015 uliofanyika juzi katika Viwanja vya
Shule ya Msingi Kiwanga cha Ndege Morogoro, viongozi wengi wa chama
hicho akiwamo Katibu Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar, Maalim Seif Shariff Hamad, walimnadi Prof Lipumba
jukwaani wakidai kuwa bado ni kiongozi anayestahili kugombea wadhifa
huo kupitia CUF.
Awali kabla ya kufanyika kwa mkutano huo
uliopambwa na shamra shamra za ngoma zilizoanza siku mbili kabla ya
uzinduzi huo zikiambatana na baadhi ya wafuasi na wapenzi wa chama hicho
kupita katika mitaa mbalimbali ya mji wa Morogoro wakiperusha bendera,
uliingia dosari baada ya kutanguliwa na mvua kubwa iliyokwamisha baadhi
ya shughuli na kuchelewa kuanza kwa mkutano huo.Kwa habari zaidi bofya na Endelea....>>>>