EBONY FM YASHEREHEKEA VALENTINE DAY KIHIVI.........

 
  Bw. Raymond Francis mratibu wa zoezi hilo, na mtangazaji wa kituo cha Radio Ebony fm akitoa nasaha juu ya harambee na siku ya Wapendanao- VALENTINE DAY, katika hafla ya kukabidhi misaada kwa watoto yatima.
 Baadhi ya watoto yatima wa kituo cha "Sisi ni Kesho"
 
WAKATI akili, Mioyo na fikra za wananchi walio wengi duniani kote zikielekezwa katika siku ya wapendanao almaarufu kama “VALENTINE DAY” kama ni siku ya kimahaba na kimapenzi,  mambo hayo yamekuwa tofauti kwa wakazi wa mikoa ya nyanda za juu kusini- Iringa, Mbeya..

Hatua hiyo imekuja baada ya radio Ebony fm iliyopo katika mkoa wa Iringa kubadili mfumo na utaratibu huo, na hivyo kuwahamasisha wananchi kuchangia ili kuwatembelea kundi la watu wenye mahitaji muhimu.

Akizungumzia mpango huo, mratibu wa zoezi  la hilo lenye kaulimbinu ya “VALENTINE DAY 2013, UPENDO KWA WATOTO” kupitia kampuni ya Ebony fm, Bw. Reymond Fransis Chali - amesema lengo la kuendesha harambee hiyo ni kuwakumbuka watu wenye mahitaji muhimu ambao wamesahaulika katika jamii, hasa katika siku hiyo ya wapendanao.

“Imezoeleka kama siku hii ya VALENTINE ni malumu kwa wapenzi, katika kununuliana kadi, Maua mekundu, na zawadi mbalimbali, fikra hizi kupitia kituo chetu cha Ebony nikaamua kubadili mawazo hayo na hivyo kuwaelekeza wananchi kuwakumbuka watoto yatima na wale wanaoishi katika maisha magumu na hatarishi,” Amesema Reymond.

Aidha Reymond amesema anawashukuru wananchi wote waliopokea kwa mikono miwili zoezi hilo na kwa kuitikia harambee hiyo ya uchangiaji wa fedha na mahitaji mbalimbali kwa watoto wa kituo cha “SISI NI KESHO” kilichopo kijiji cha Nyololo katika Wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa.

Amesema jumla ya fedha zilizochangwa na wananchi kupitia M-PESA ni zaidi ya shilingi Milioni 9.5, huku baadhi ya wananchi wakijitolea kwa hali na mali vifa mbalimbali kama Magodoro zaidi ya 15, nguo, mashuka, Mablanketi, Viatu, Vinywaji baridi (Visivyo na kileo), Katoni za Sabuni, Sukari, Unga wa ugali na Ngano, madishi ya kufulia na kuogea na hata mabero ya nguo mbalimbali.

Ofisa tawala wa Wilya ya Mufindi Bi. Maria Waitara ameitaka jamii kuiga mfano huo, kwa kuyakumbuka makundi hayo, hasa hilo la watoto yatima ambao kwa kiwango kikubwa wamepoteza wazazi wao kwa tatizo la ugonjwa wa ukimwi.

“Kwa kweli Radio Ebony imetupa somo, kubadili sura ya siku ya VALENTINE kwa kuwakumbuka watoto hawa, tunatakiwa kuendeleza zoezi hili ambalo katika wilaya yetu limetusaidia, kwani watoto hawa ni wetu wote, kuna watu watu wanafanya maasi mengi katika siku kama hii, lakini hawa ndugu zetu wameamua kuleta misaada hii ambayo itawasaidia kwa muda mrefu watoto wetu,” Alisema Waitara.

Hata hivyo Bi. Suzana Mfugale mmoja wa wahudumu wa kituo hicho cha “SISI NI KESHO” akisoma lisara  katika hafla hiyo amesema changamoto inayokikabiri kituo hicho ni pamoja na jamii kutojihusisha katika kuhudumia watoto hao, na hivyo kuwepo kwa mapungufu mengi.
 
source:Olivermoto blog


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo