UPUNGUFU WA DAWA HOSPITALI YA TUMAINI WAWASHTUA MADIWANI

 
Madiwani wilayani Hanang’ mkoani Manyara wamelalamikia upungufu mkubwa wa Dawa na ukosefu wa huduma za Afya katika Hospitali ya Tumaini iliyoko maeneo ya Katesh wilaya ya Hanang’ mkoani Manyara.
 
Malalmiko hayo yamekuja kutoka kwa baadhi ya madiwani wa Halmashauri hiyo kwenye kikao cha Baraza la madiwani la kujadili taarifa ya utekelezaji kwa kipindi cha robo mwaka ya pili Oktoba hadi Desemba 2012.
 
Naye Diwani wa Kata Endagaw Hassan Hilbagroy aliuliza kuwa sifa ya vituo vya Afya ni zipi?ni mlundikano wa wagonjwa au ni mahali pa kupatia tiba ?wakati akichangia hoja yake kuhusu ukosefu wa huduma stahili katika Hospitali na vituo vya afya wilayani hapo.
 
Alisema kuwa kuwasilisha kwa masikitiko hayo kwa kusema mgonjwa anafika kwenye kituo cha Afya atakaa hapo akisubiri kumwona mganga kwa zaidi ya masaa matatu,akiandikiwa dawa anaenda tena kukaa kwa masaa matatu kumsubiri mtoa dawa, mtoa dawa akifika anasema dawa hakuna,huu ni mchezo gani.
 
Naye mganga mkuu wa Wilaya ya Hanang’ Dr Philemon Kiambile wakati akijibu hoja hiyo kwa madiwani hao amekiri kuwepo kwa upungufu wa Dawa na kueleza kuwa upungufu huo umetokana na uchangiaji mdogo wa mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) .
 
Aidha kijibu hoja hizo kwa madiwani hao alisisitiza kuwa tayari Halmashauri ya wilaya hiyo imepokea ruzuku kutoka Serikalini ya kiasi cha Tshs milioni 44 kwa ajili ya ununuzi ya Dawa ambazo zitasambazwa kwenye vituo vyote vya Afya pamoja na Zahanati.
 
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Wilaya ya Hanang’ Filex Mabula ameagiza iundwe timu itakayofanya ununuzi wa dawa kwa uwazi na kusambazwa kwa uwazi ili hata wananchi wajue kwamba kituo kina madawa.
 
Alisema kuwa wanataka ununuzi wa madawa ufanyike kwa uwazi ili hata wananchi wao wajue dawa kwenye kituo chao zipo,hata akienda kutibiwa akiambiwa hakuna dawa awe na maswali ya kuhoji yameenda wapi iwapo ni wiki tu tangu ziletwe.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo