Marubani wa Shirika la
Ndege la Tanzania (ATCL) wakiwa wanafanya ukaguzi wa mwisho kabla ya
kuanza safari ya kutoka Kigoma kuenda Dar es Salaam leo asubuhi. Hii ni
baada ya wahandisi wa shirika hilo kukamilisha kufunga kioo kipya
ambacho kimenunuliwa kutoka nchini Marekani. Ndege hii aina ya Dash-8
Q300 yenye namba za usajili SH-MWF ambayo ilisitisha safari zake za
Kigoma baada ya kioo cha mbele katika chumba cha marubani kupata ufa
(Wind shield crack) tarehe 11 Januari, 2013, muda mfupi baada ya
ndege hiyo kuruka kutoka
Kigoma kurudi Dar Es Salaam katika safari zake za kawaida, imeanza tena
safari za Dar-Kigoma-Dar kulingana na ratiba .
Ndege hiyo leo imetua katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa
Julius Nyerere ikitokea Kigoma ikiwa imebeba abiria 22.
Uongozi wa Shirika imedhibitisha kuwa safari za
Dar-Kigoma-Dar zitaendelea kama ratiba inavyosema.
Abiria wakipanda ndege ya
Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika uwanja wa ndege wa Kigoma,
tayari kwa safari ya kuelekea Dar es Salaam.