MWILI WA MWANAMKE ANAYEDAIWA KUUAWA WAOKOTWA KORONGONI

Mwanamke anayejulikana kwa jina  Mwanaisha Idd umri wa miaka 25 mkulima wa kijiji cha Kichameda amekutwa ameuwawa  kwenye korongo   eneo la Mrara mjini Babati mkoani Manyara. 
 
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa polisi wa mkoa wa manyara Akili Mpwapwa alisema kuwa tukio hilo lilitokea januari 10 mwaka huu majira ya saa 11 jioni marehemu alikutwa amekufa korongoni huku mwili wake ukiwa uchi huku nguo zake zikiwa pembeni mwake. 
 
Aidha aliongeza kuwa mwili wa marehemu Mwanaisha umekutwa amechuchumaa kama akisujudu huku akiwa ameingiliwa kimaumbile pande zote mbili hakuwa na jereha lolote lile. 
 
Kamanda Mpwapwa aliendelea kusema kuwa kutokana na tukio hilo uchunguzi umefanywa na kuweza kumkamata mtu mmoja ambaye alizaa na marehemu watoto wawili anayeitwa John Mathayo umri wa miaka 35,mkulima wa kijiji cha Kichameda. 
 
Alisema kuwa John Mathayo alikuwa na mahusiano na marehemu mwanaisha ambapo yupo mtuhumiwa amekamatwa na yupo ndini kwaajili uchunguzi, atafikishwa mahakamani  upelelezi ukikamilika.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo