WATU SABA KIZIMBANI KWA KOSA LA KUHUJUMU UCHUMI MKOANI MANYARA

 
Elephants - 
Tarangire National Park
WATU watatu wamefikishwa Mahakamani   Mkoa wa Manyara wakishtakiwa kwa kosa la uhujumu uchumi kwa kuua tembo na kosa la jinai la kukutwa na silaha wakati wakiwinda wanyamapori katika hifadhi ya Tarangire.
 
Aidha  wakisomewa mashtaka hayo  mjini Babati mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Rashid Chaungu, mwendesha mashtaka Linus Bugaba alisema kuwa  washtakiwa hao wanadaiwa kutenda makosa hayo Agosti 27 mwaka jana.
 
Amewataja washtakiwa hao kuwa ni Gidabijo Gidabungeta (35) mkazi wa Makuyuni mkoani Arusha,Mahaya Gidamude (26) na Masanja Bajuta (26) wote wakazi wa kijiji cha Mdori wilayani Babati mkoani Manyara. 
 
Aliendelea kusema kuwa katika kesi namba 21/2012 ya uhujumu uchumi washtakiwa hao wanadaiwa kumuua tembo mmoja na kisha kuchukua pembe zake na kesi ya jinai namba 441/2012 wanadaiwa kukutwa na silaha ya bunduki na risasi.
 
Alisema kuwa  kwenye shtaka la kwanza ya uhujumu uchumi,washitakiwa hao wanadaiwa kukutwa na nyara za Serikali baada ya kumuua tembo mmoja na kuchukua pembe zake ambazo juzi zililetwa Mahakamani hapo kama kielelezo.
 
Bugaba alibainisha kuwa  shtaka la pili linalowakabili washtakiwa hao ni kukutwa kwenye tukio hilo hifadhi ya Tarangire wakiwa na silaha aina ya Rifle 404 risasi mbili za 404 na maganda yake,mkuki na kielelezo cha nguo (shuka za kibarabaig). 
 
Kwa upande wao washtakiwa hao wamekana makosa hayo na wapo nje kwa dhamana hadi Januari 31 mwaka huu ambapo kesi ya jinai upande wa mashtaka wataendelea na ushahi wao pamoja na kuonyesha vielelezo.
 
Aidha  Bugaba alimalizia kwa kusema   kuwa kosa la uhujumu uchumi lipo kwenye hatua ya kutajwa kwani wanasubiri kibali kutoka kwa mwanasheria wa Serikali na itajawa Januari 31 mwaka huu.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo