MTENDAJI ATUHUMIWA KWA WZI WA MAHINDI


WANANCHI wa kijiji cha Bugwema wilayani Butima mkoani Mara,wamemtuhumu mwenyekiti wa kijiji hicho kuiba Mahindi ya msaada ambayo yametolewa na serikali kwaajili ya kukabiliana na njaa huku akiwalinda wezi wa mifugo katika kijiji hicho.
 
Wananchi hao wametoa tuhuma hizo katika mkutano wa hadhara mbele ya mkuu wa mkoa wa Mara Bw John Tupa,ambayo amekuwa akiifanya katika vijiji mbalimbali kwaaji ya kutafuta njia sahihi ya kukabiliana na uhalifu yakiwemo mauaji ya kinyama katika wilaya hiyo.
 
Hata hivyo mwenyekiti huyo wa Serikali ya kijiji hicho Bw Johanes Sando,amekiri kuwepo kwa tuhuma hizo ambapo amesema tayari zimefikishwa polisi ili kuona kama zina ukweli wowote huku mwenyekiti wa CCM wa wilaya hiyo Bw Yahona Mirumbe akivitaka vyombo vya dola kuchukua hatua kwa kiongozi yoyote bila kujali cheo chake ambaye atabainika kujihusisha vitendo viovu vikiwemo wizi na mauaji.
 
Kwa upande wake mkuu huyo wa mkoa wa Mara John Tupa,akizungumza katika mkutano huo wa hadhara ametoa wiki moja kwa viongozi na watu wote wanajihusisha katika mtandao wa wizi wa mifugo kujisalimisha wenyewe mara moja kwa mkuu wa polisi wilaya kabla ya jeshi la polisi kuwamata na kuwafikisha katika vyombo vya sheria.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo