Mstahiki
Meya wa Manispaa ya Ilala ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Gongo la
Mboto Jerry Silaa akisani kitabu cha wageni wakati wa Halfa fupi ya
uzinduzi wa mradi wa maji wa Pugu Kajiungeni. Kushoto ni Diwani wa kata
ya Pugu Kajiungeni Emelda Samjela.
Diwani
wa kata ya Pugu Kajiungeni Emelda Samjela akizungumza na wakazi wa Kata
yake kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Mstahiki Meya wa Manispaa ya
Ilala Jerry Silaa.
Mstahiki
Meya wa Manispaa ya Ilala ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Gongo la Mboto
Jerry Silaa akitoa taarifa wakati akizindua Mradi wa Maji Pugu
Kajiungeni ambapo amesema mradi huo unatokana na kisima cha maji chenye
urefu wa mita 122 toka usawa wa ardhi.
Mstahiki
meya amesema kisima hicho kina uwezo wa kuzalisha maji kiasi cha lita
60,000 kwa saa. Ameongeza kuwa mradi huo utakuwa na mtandao wa mabomba
wa kilometa 9, vituo 25 vya kuchota maji, nyumba ya pampu, fensi pamoja
na uzio.
Aidha
amewataka wananchi wa maeneo husika ya Pugu Kajiungeni ni kuitunza
miradi hii na kutoa ushirikiano kwa wakandarasi ili kuweza kufanikisha
malengo yaliyokusudiwa. Kushoto ni Diwani wa Kata ya Pugu Emelda Samjela
na wa pili kulia ni Mwenyekiti wa CCM Kassim Mjesa na Kulia ni
Mkandarasi wa Kampuni ya Meero Contractors ltd inayoshughulikia mradi
huo Method Mlay.
Pichani
Juu na Chini ni baadhi ya wakazi wa Kata Pugu Kajiungeni watakaofaidika
na mradi huo wakimsikiliza mstahiki Meya Jerry Silaa (hayupo pichani).
Mstahiki
Meya wa Manispaa ya Ilala ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Gongo la Mboto
Jerry Silaa akimkabidhi Mkandarasi wa Kampuni ya Meero Contractors ltd
Method Mlay (kulia) barua rasmi ya mradi wa maji wa Pugu Kajiungeni
unaotekelezwa kwa ushirikiano na wahisani /wafadhili wa Serikali ya
Ubelgiji, Umoja wa Ulaya (EU), Serikali ya Tanzania, Halmashauri ya
manispaa ya Ilala na wafadhili wengine mbalimbali. Anyeshuhudia tukio
hilo ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Ilala Kassim Mjesa.
Mkandarasi
wa Kampuni ya Meero Contractors ltd Method Mlay (kulia) akitoa neno la
shukrani baada Mstahiki Meya kumkabidhi barua rasmi ya ujenzi wa mradi
wa maji wa Pugu Kajiungeni na kuahidi kutoa ajira kwa Vijana wa maeneo
ya Pugu kuanza sasa mpaka mradi utakapokamilika.
Mstahiki
Meya Jerry Silaa akipongezwa na wakazi wa Pugu baada ya kuzindua rasmi
mradi wa maji wa Pugu Kajiungeni ulioanza kubuniwa rasmi mwaka 2011.