MAPOKEZI YA MANGULA IRINGA YATIKISA MJI

Wanachama  wa CCM tawi la  chuo  cha Mkwawa  wakiwa na mabango mkatika mapokezi ya mangula leo

Umati  wa  wana CCM waliofika  uwanja wa Mwembetogwa  kumsikiliza Mangula
Makamu  mwenyekiti  wa CCM bara Philip mangula katikati akiwa na mwenyekiti  wa CCM mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu na mwenyekiti  wa CCM wilaya ya Iringa mjini Abed Kiponza  kulia
  Na Francis Godwin
MAPOKEZI  makubwa  ambayo ameyapata  makamu  mwenyekiti  wa  chama  cha mapinduzi (CCM) Tanzania bara Philip Mangulla yametishia  uhai  wa  chama  cha Demokrasia na maendeleo (Chadema) jimbo la Iringa  mjini .

Huku  wanafunzi  wa  chuo  kikuu  kishiriki  cha elimu Mkwawa wakimpokea Mangula kwa mabango yenye jumbe mbali mbali ukiwemo  wa  kumpongeza Mangula kwa kuteuliwa na ule  unaolalamikia utaratibu mbovu  wa ucheleweshaji  wa mikopo kwa  wanafunzi hao  wa vyuo  vikuu pamoja na kuitaka  CCM kukomesha  vitendo  vya rushwa ndani na nje ya chama.

Katika historia  ya CCM jimbo la Iringa na mkoa  wa Iringa haijapata  kutokea mapokezi ya kishindo kama hayo baada ya umati mkubwa  wa  wananchi kujitokeza  kumpokea Mangula huku maeneo mbali mbali  ya mji  wa Iringa yakipambwa  kwa  bendera  za CCM mithiri ya makao makuu ya CCM Dodoma wakati  wakati  wa  mkutano mkuu  wa chama  hicho.

Wakizungumzia  juu ya mapokezi hayo ya kishindo kwa Mangula baadhi ya  wananchi  wameonyesha kutofautiana  juu ya mapokezi hayo  huku baadhi yao  wakidai kuwa maandalizi ya mapokezi hayo yamefanywa na Jesca Msambatavangu ambae ni  mwenyekiti  wa CCM mkoa  wa Iringa ambae ni mwanamke  wa kwanza  kuongoza  chama  hicho toka nchi  ilipopata  uhuru  wake  mwaka 1961 huku  wengine  wakidai kuwa ni matokeo ya kukubalika kwa sekritaeliti mpya  ya CCM akiwemo katibu mkuu  wa CCM na mwenyekiti na makamu  wake bara na visiwani.

Katibu  wa  umoja  wa vijana  wa CCM mkoa wa Iringa Rhoda George alisema  kuwa wananchi wa  jimbo la Iringa mjini  wamejitokeza  kwa  wingi katika mapokezi hayo  kutokana na utekelezaji mzuri  wa Ilani ya CCM unaofanywa na madiwani  wake pamoja na  wabunge  wa  CCM mkoa  wa Iringa.

Hata  hivyo  alisema  kuwa  mapokezi  hayo makubwa  kwa  wananchi  wa  jimbo la Iringa mjini ni ishara nzuri  ya ushindi  wa CCM katika  uchaguzi  wa  serikali za mitaa pamoja na uchaguzi mkuu mwaka 2015 katika  jimbo  hilo.

Kwa  upande  wake Brown Payovela alisema  kuwa  wakazi  wa mkoa  wa Iringa  wameonyesha matumaini makubwa  kwa Mangula na kuwa upo uwezekano mkubwa  wa CCM kuendelea  kushinda kwa  kishindo katika chaguzi  zake  zijazo.

Baadhi ya wananchi mashabiki  wa vyama vya upinzani mjini Iringa walisema  kuwa CCM imetumia mbinu ya kunyong'onyeza  nguvu ya vyama  vya upinzani katika  jimbo  hilo la Iringa mjini hasa chama cha Chadema ambacho mbunge wake  ni mchungaji Peter Msigwa .

Hivyo  walisema  kuwa iwapo mbunge  wa  jimbo  hilo Mchungaji Msigwa hatafanya kazi zinazoonekana  uwezekano  wa  kuambulia kura mwaka 2015  unaweza  kuwa mdogo japo  walisema  kuwa  katika uchaguzi mkuu mwaka 2015 upinzani bado utategemea huruma za wana CCM kuendelea  kumchagua mbunge  huyo ila iwapo CCM itafanya mchezo mchafu katika utaratibu  wa  kumpata mgombea wa ubunge  jimbo  hilo.

Alisema Damas Kalinga mkazi  wa Kihesa ambaye alijitambulisha kuwa ni shabiki  wa Chadema kuwa hadi  sasa ndani ya CCM jimbo la Iringa mjini tayari  wagombea  wameanza  kuwachanganya  wananchi kwa  kila mmoja kuonyesha  kuitaka nafasi  ya ubunge na kuwataka  viongozi  wa CCM kuwa makini  zaidi.

Miongoni  mwa  wabunge  waliojitokeza katika mapokezi hayo ni pamoja  na mbunge  wa  viti maalum mkoa  wa Iringa Ritta kabati , mbunge  wa  jimbo la kalenga na  waziri  wa fedha Dr Wiliam Mgimwa,makada  wa CCM pamoja na wakuu  wa wilaya za Iringa , Kilolo na Mufindi wakiongozwa na mkuu wa mkoa  wa Iringa Dr Christine Ishengoma.

Kwa  upande  wake mwenyekiti  wa CCM mkoa  wa Iringa Jasca Msambatavangu  akimkaribisha Mangula katika uwanja  huo  wa Mwembetogwa kwa ajili ya  kuwahotubia  mamia ya  wananchi  waliofika katika  uwanja  huo alisema  kuwa CCM itaendelea  kueleza  utekelezaji  wa Ilani ya uchaguzi kwa  wananchi  wake na  kuwa tayari baadhi ya kata  zimeanza  kutoa utekelezaji  wa ilani  hiyo kwa  wananchi.

Msambatavangu aliwapongeza  wanachama wa vyama vya upinzani ambao  wameanza  kurudi CCM na  kuwa  kurejea kwa wanachama hao  wa vyama vya upinzani ndani ya CCM ni kutokana na utekelezaji mzuri  wa ilani yake kwa  wananchi na uendeshaji wa CCM ndani ya CCM bila kunadi sera  za matusi na ubaguzi .


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo