JK AOMBWA KUINGILIA KATI MGOGORO WA MPAKA KIJIJI CHA SUKURO

DSCF7301
Mwenyekiti wa kitongoji cha  Mowalak kijiji cha Sukuro wilayani Simanjiro mkoani Manyara,Lengai Ole Makoo akilaani kitendo cha baadhi ya viongozi wa serikali na kisiasa wilayani humo kwa kuwakamata hovyo na kisha kuwabambikia kesi baadhi ya viongozi wa kijiji hicho juzi katika mkutano ulioitishwa na serikali ya kijiji hicho,kushoto kwake ni mwenyekiti wa kitongoji hicho,Kaayai Murero(picha na habari na Jamii blog http://pamelamollel.wordpress.com

WANANCHI wa kijiji cha Sukuro wilayani Simanjiro mkoani Manyara wamemwomba Rais Jakaya Kikwete aingilie kati sakata la mpaka kati ya kijiji chao na Kitiengare kilicho dumu kwa muda mrefu bila kupatiwa ufumbuzi huku wakisema kuwa wamechoka kunyanyaswa kwa kukamatwa mara kwa mara na kisha kubambikiwa kesi  mbalimbali viongozi wao jambo ambalo linapelekea wao kukosa maendeleo

Pia,wamemtupia lawama mbunge wa jimbo hilo Christopher Ole Sendeka kwa kutowasaidia katika mgogoro huo sanjari na kusikitishwa na kauli zake kwamba mgogoro huo umeshamalizika huku wakidai nijambo ambali halijapatiwa ufumbuzi bado
 
Wakizungumza kwa nyakati tofauti  katika mkutano ulioitishwa na uongozi wa serikali ya kijiji hicho kujadili tukio la kukamatwa kwa viongozi wa serikali ya kijiji hicho pamoja na viongozi wa chama  cha mapinduzi hivi karibuni walionyesha kutoridhishwa na viongozi wa serikali Mkoani hapo“Hatuna imani na viongozi wetu wa  serikali pamoja na mbunge wetu,,,tumeendelea kunyanyaswa hadi kufikia kukamatwa kwa viongozi wetu wa kijiji jambo ambalo limezidi kukutesa sana hapa kijijini”sauti ilisikika katika mkutano huo
 
Akizungumza katika mkutano huo,mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho,Kaayai  Murero alisema kwamba hivi karibuni baadhi ya viongozi wa serikali ya kijiji hicho akiwemo yeye pamoja na viongozi wa chama cha Mapinduzi(CCM) walikamatwa na jeshi la polisi na kisha kuachiwa katika mazingira ya kutatanisha.
 
Alisema kuwa kumekuwa na hali ya wasiwasi kijijini kwao kwa kuwa baadhi ya familia zinaishi kwa hofu kutokana na mgogoro wa ardhi baina ya kijiji chao na Kitiengare kwa kuwa wamekuwa wakikamatwa hovyo na jeshi la polisi wilayani humo na kisha kubambikiwa kesi.
 
Mwenyekiti huyo kwa unyonge alimuomba  Rais Kikwete kuingilia kati mgogoro huo huku akidai kuwa umedumu kwa muda mrefu na uongozi wa serikali na chama cha CCM mkoani Manyara hauonyeshi jitihada za dhati kuutatua mgogoro huo.
 
Naye,mwenyekiti wa kitongoji cha Molawak,Lengai Ole Makoo alisema kuwa baadhi ya wananchi waekuwa wakikamatwa hovyo na jeshi la polisi kwa madai ya kuchangia fedha za kuendesha kesi iliyopo mahakamani kwa lengo la kudhoofishwa ili wasipate mwanya wa kuendelea na kesi hiyo
 
Alisema kuwa  wananchi hao wamekuwa wakipigwa na kutishiwa kunyang”anywa kadi za CCM kwa madai kwamba  waachane na kesi ya kudai ardhi  waliyoifungua mahakamani wilayani Babati na kumtaka Rais Kikwete aingilie kati.
 
Nao baadhi ya wakazi wa kijiji hicho,Abraham Koringo,Olais Soyai na Magdalena Daniel walimwomba Rais Kikwete kuwasaidia katika unyanyasaji huo huku wakidai kwamba wamekuwa wakihangaishwa kwa muda mrefu kama wao ni wakimbizi katika nchi yao
 
Hata hivyo walisisitiza kwamba baadhi ya wanasiasa pamoja na viongozi wa serikali hawana nia njema ya kuutatua mgogoro huo uliodumu kwa takribani miaka mitano kwa kuwa wananufaika kwa kupokea chochote.
 
“Tunaitaka serikali ifanye maamuzi magumu tunamwomba mheshimiwa Rais aingilie kati kwa kuwa vijiji vya Kitiengare na Sukuro vilitenganishwa kisheria sasa hii leo tunataka kunyang”anywa ardhi yetu”walisema kwa unyonge wananchi hao
 
Pia Katika mkutano huo baadhi ya wazee wa mila maarufu kama Malaigwanani walihudhuria mkutano huo ambapo kwa sauti ya pamoja walitoa tamko la kuendelea kuchangishana fedha za kugharamia kesi waliyoifungua mahakamani kudai ardhi ndani ya kijiji chao.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo