AMTUPA MWANAYE CHOONI ILI ASIKOSE BWANA!

MKAZI mmoja wa Kijiji cha Mnazi kilichopo Kata ya Ulumi wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa, Prisca Dickson mwenye umri wa miaka 17, anashikiliwa na polisi kwa tuhuma ya kutupa mtoto wake chooni mara baada ya kujifungua, kwa hofu ya kuachwa na mchumba wake.
 
Taarifa zinasema kuwa, mtoto huyo wa siku moja ametupwa katika choo cha jirani, akiwa ameviringishwa katika kipande cha kanga. Kamanda wa Polisi mkoani Rukwa, Jacob Mwaruanda amesema kuwa, Prisca amemtupa mtoto huyo mara baada ya kujifungua, na kusababisha kifo chake kutokana na kukosa hewa ambapo mwili wa kichanga hicho umegunduliwa na wanafunzi wa Shule ya Msingi Mnazi ambao walipita asubuhi katika nyumba hiyo ya jirani na mmoja wao aliingia chooni kujisaidia na kukuta maiti hiyo ikielea kisha alitoa taarifa. 
 
 Kamanda Mwaruanda amesema kuwa, baada ya uchunguzi imebainika kuwa Prisca ndiye aliyefanya kitendo hicho. Ameongeza kuwa, binti huyo amedai kuwa imemlazimu kufanya hivyo kwa kuwa, ujauzito aliokuwa nao ni wa mwanaume mwingine. Mtuhumiwa anatarajiwa kufikishwa mahakamani mara baada ya kukamilika kwa uchunguzi wa tukio hilo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo