KERO ZA WANANCHI ZAMSABABISHA MKUU WA MKOA WA NJOMBE KUFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA


Na Riziki Manfred

Mkuu wa mkoa wa Njombe Kepteni mstaafu Asery Msangi amefanya ziara ya kushtukiza katika shamba la ngano lililoko kijiji cha Ludodolelo kata ya Mang’oto wilaya ya Makete baada ya kupata malalamiko kutoka kwa wananchi wanaozunguka shamba hilo

Mkuu huyo wa mkoa amefanya ziara hiyo hii leo akiwa ameongozana na mkuu wa wilaya ya Makete Bi Josephine Matiro pamoja na viongozi wengine ili kujionea uendeshwaji wa shamba hilo ambalo baadhi ya wananchi wamekuwa wakilalamikia uendeshwaji wake

Shamba hilo linalomilikiwa na kampuni ya SELUE COMPANY LIMITED limelalamikiwa na wakazi wa eneo hilo kwa madai kume kuwa na umwangaji wa dawa ya kuuwa magugu shambani wakati wauandaaji wa mashamba hayo na dawa hiyo inayosadikika kuwa ni sumu imekuwa ikisambaa katika mashamba ya wakazi hao na  kuharibu mazao ikiwemo miti pamoja na uchafuzi wa vyanzo vya maji

Wameeleza kuwa dawa hiyo imekuwa ikitiririka hadi kwenye chanzo cha maji kinachopeleka maji kwenye kijiji chao na Njombe mjini jambo ambalo ni hatari kwa watumiaji wa huduma hiyo.

Aidha kabla ya kufanya ukaguzi katika shamba hilo mkuu wa mkoa aliongea na mmoja wa wasimamizi wa shamba hilo ambaye alikiri kutumia  dawa hiyo ambapo amesema wamekuwa waangalifu pindi wanapo mwaga dawa hiyo kwani wanatambua umuhimu wa afya za binadamu na wamekuwa wakishirikisha wataalamu wakati wa umwagaji dawa hiyo na kukanusha malalamiko ya wananchi kuwa si kweli.

Baada ya kupokea taarifa hiyo mkuu wa mkoa pamoja na msafara wake walielekea kukagua shamba hilo ambapo hawakuona mazao wala miti iliyoathiriwa na dawa hilo jambo ambalo liliibua maswali mengi kwa mkuu wa mkoa na kutaka kujua uhusiano uliopo kati ya mwekezaji huyo na wananchi wanaozunguka eneo hilo.

Katika hatua nyingine mkuu wa mkoa amemtaka mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya Makete kuwa karibu na wawekezaji waliopo wilayani mwake kwani kufanya hivyo kutasaidia  kudhibiti mapato ya halmashauri ili kufikia malengo yanayokusudiwa na serikali



JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo