Mbunge Filikunjombe (kushoto)
akimchana diwani wa kata ya Madope Bw Mhagama (kulia) katikati ni
mwenyekiti wa CCM wilaya Bw Kolimba akisikiliza kwa umakini
Na Francis Godwin
KATIKA hali
isiyotegemewa mbunge wa jimbo la Ludewa mkoani Njombe Deo Filikunjombe (CCM)
amemkataa mbele ya viongozi wa CCM
na wapiga kura
diwani wa kata ya Madope jimbo la Ludewa kupitia chama cha mapinduzi
(CCM) Godfrid Mhagama kwa madai kuwa ni
diwani anayeongoza kwa kumdanganya yeye kama mbunge pamoja na wapiga
kura wa kata hiyo.
Mbunge
Filikunjombe alisema kuwa
diwani huyo amekuwa ni mmoja kati ya watu
wanaoeneza chuki ya ukabira
katika kata hiyo kwa kuwabeza viongozi wa
wilaya na mbunge kutokana na
kuwa si wenyeji wa kata
hiyo ni watu kutoka ukanda wa ziwani jambo ambalo ni hatari kwa
maendeleo ya kata hiyo iwapo
siasa za ukabira na ukanda zitapewa nafasi.
Akizungumza katika mkutano maalum kijijini hapa mara baada ya
kufunguza ofisi ya chama cha ushirika wa kuweka na kukopa ya Farasa
Saccos ,juzi Filikunjombe
alisema kuwa moja kati
ya kata ambazo madiwani wake
toka walipochaguliwa mwaka 2010 hawafanyi kazi ya kimaendeleo na badala
yake wamekuwa wakieneza
chuki ya kuwagawa viongozi na
wananchi ni pamoja na kata hiyo
ya Madope ambapo diwani amekuwa akiendesha majungu mitaani na kuacha kusimamia shughuli za kimaendeleo.
Alisema kuwa diwani huyo amekuwa ni kikwazo kikubwa ndani ya CCM kutokana na kushindwa
kusimamia ujenzi wa
shule ya Msingi Mangalanyena ,kushindwa
kusimamia ujenzi wa Zahanati katika kijiji
hicho pamoja na ujenzi wa
barabara na kila anapoulizwa amekuwa
akitoa majibu ya uongo mbele yake .
Mbunge huyo alisema katika
hali ya kushangaza diwani
huyo baada ya kuulizwa mkakati
wa kata katika kusimamia ujenzi wa Zanahati ya kata
kijijini hapo alieleza kuwa
mkakati wa ujenzi huo na miradi mingine
iliyosimama katika kata yake ya Madope imeingizwa katika kipindi cha fedha cha mwaka 2013 /2014 bajeti huku
akitambua kuwa huo ni uongo kwani bajeti
ya mwaka wa fedha wa 2013/2014 bado
kupitishwa.
Hata hivyo alisema kupitia diwani
huyo kata hiyo wamekuwa
wakiwachukia viongozi wa chama na
serikali ambao si wa kabila la
kwao huku wakiendelea kukwamisha miradi ya maendeleo katika
kata hiyo kama njia ya kuwafanya
wananchi waungane nao katika
kuwachukia viongozi wa wilaya
hiyo .
“Nimechukizwa sana na
tabia ya mheshimiwa diwani wa kata
hii Bw Mhagama kwa kushindwa kufanya kazi za kimaendeleo badala yake
anashinda vijiweni kuwaelewa
wananchi uongo juu ya viongozi
kuwa si
wa ukanda wao …..nasema diwani
kama unataka kuendelea kuendesha uongo
na kushindwa kufanya kazi yako ni vema
ukakaa pembeni ili wananchi
waendelee kujiletea maendeleo….nchi
yetu na chama chetu hatuchaguani kwa
ukabila wala rangi tunachangana
kwa uwezo wa mtu na utendaji sio hivyo
unavyofanya wewe”huku akishangiliwa na
wananchi waliofika katika mkutano huo
Filikunjombe aliwataka
wananchi kutomsikiliza diwani
huyo iwapo atashindwa kubadilika
na kuendelea kueneza
chuki katika kata hiyo kati
ya viongozi wa juu wa
wilaya na jimbo na wananchi wake .
Wakati kwa upande
wake diwani Mhagama alipofuatwa
na mwandishi wa habari hizi ili kujibu
tuhuma hizo dhidi yake alisema
kuwa si kweli kama amekuwa akieneza
siasa za ukabila katika kata hiyo na
kuwa wanaofanya hivyo ni watu baki na
sio yeye kama ambavyo mbunge amekuwa akimtuhumu .
Kuhusu kukwama kwa
miradi ya kimaendeleo katika kata yake ya Madope alisema kuwa
kutokana na maelekezo ya mbunge
atahakikisha anakuwa mbele katika kusimamia miradi hiyo na kuwa kwa upande wake amekuwa akikwamishwa na watendaji
wa Halmashauri ambao
wamekuwa hawafiki kufanya ukaguzi wa miradi katika kata hiyo.
Katika hatu
nyingine mbunge Filikunjombe ameahidi kusimamia ujenzi wa zahanati
hiyo hadi ukakapokamilika ili
kuwawezesha wananchi hao wa kupata
huduma ya afya jirani zaidi.