ETI AROBAINI YA CHADEMA NDIYO HII


Na Charles Charles
“KUZUNGUKA huku na huko kwa CCM ni kutuiga sisi. 
Tumeanza muda mrefu baada tu ya uchaguzi mkuu 
wa mwaka 2010”, ndivyo anavyosema Katibu Mkuu wa 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), 
Dk. Willibrod Slaa.
Anaongeza kwamba “Chadema ni mwalimu” huku Chama 
Cha Mapinduzi (CCM) kikiwa mwanafunzi anayefuata 
nyayo kwa mambo yanayofanywa na chama chake hicho. 
Alikuwa akizungumza na gazeti moja la kila siku 
nchini kufuatia ziara iliyofanywa hivi karibuni na Katibu 
Mkuu wa CCM, Kanali Abdulrahman Kinana katika 
mikoa minne ya Arusha, Geita, Mtwara na Rukwa.
Siku chache baadaye, yeye mwenyewe alifanya ziara 
katika majimbo matatu ya Temeke, Kigamboni na 
Kinondoni jijini Dar es Salaam na kukumbana na hali
 ngumu kuliko wakati wote uliopita.
Tatizo hilo liliambatana na ‘kudoda’ kwa harambee 
ya kuchangia kile kinachoitwa kuwa ni Vuguvugu 
la Mabadiliko (M4C) iliyofanyika jijini Mwanza, na 
kukitia chama hicho hasara ya shilingi milioni tisa.
Wakati hayo yakiendelea, Katibu wa Halmashauri Kuu 
ya Taifa (NEC) ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye 
aliibua tuhuma kwa Dk. Slaa kuwa pamoja na 
kuwashambulia sana viongozi wenzake wilayani Temeke 
akisema ni mamluki wa CCM, yeye mwenyewe ana 
kadi ya chama hicho kinachotawala, jambo alilokiri 
ni kweli na ataendelea kuitunza katika maisha yake yote.
Tayari hali hiyo imeibua mtafaruku katika chama 
chake ambapo kuna wanachama, viongozi na wafuasi 
wake hivi sasa hawana tena imani naye na kuanza 
kumtilia wasiwasi kwa kusema inawezekana pia ndiye 
anavujisha siri nyingi za Chadema kwa watu wasiohusika.
KUSOMA ZAIDI BONYEZA HAPA


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo