UNYAMA MAKETE: MAMA ATUHUMIWA KUMZIKA AKIWA HAI MTOTO WAKE!


Na Riziki Manfred, MAKETE

Jeshi la polisi wilayani Makete linamshikilia mwanamke mmoja mkazi wa Malembuli wilayani hapa kwa kosa la kumzika akiwa hai mwanaye wa kumzaa mwenyewe na kutorokakea jijini Mbeya.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo mkuu wa polisi wilaya Makete Peter Kaiza amemtaja mwanamke huyo kuwa ni Bi Fatuma Sanga mkazi wa kijiji cha Malembuli ambapo mnamo desemba 14 mwaka  huu Bi Sanga alimzika mtoto huyo akiwa hai mwenye umri wa mwezi mmoja.
 
Bwana Kaiza amesema Bi Sanga baada ya kutenda tukio hilo alitorokea jijini Mbeya na polisi baada ya kupata tarifa  kutoka kwa raia wema walilazimika kumfuata na kufanikiwa kumkamata
 
Aidha inadaiwa kuwa Bi Sanga alimzika mtoto huyo nje kidogo ya eneo analoishi ambapo alidaiwa kuwa alimzika mtoto huyo baada ya kufariki dunia lakini taarifa kutoka kwa mashuhuda zinasema huenda mtoto huyo aliuawa kabla ya kuzikwa ama alizikwa akiwa hai

Hata hivyo jeshi la polisi likuwa likimshikilia Bi Sanga pamoja na mumewe ambaye kwa sasa ameachiwa baada ya maelezo ya Bi Sanga kuwa mumewe hahusiki na wala hakujua chochote kuhusu tukio hilo

Bi Sanga anatarajiwa kufikishwa katika mahakama ya wilaya ya Makete  baada ya uchunguzi wa awali kukamilika

Hilo ni tukio la pili kutokea katika kata hiyo baada ya tukio lingine lilitokea mwaka 2009 katika kijiji cha Makangalawe ambapo mwanamke mmoja alimtupa mtoto wa siku tatu katika mto Masalala


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo