BARAZA LA WAZEE WA CCM WILAYANI MAKETE LAITAKA SERIKALI KUSIMAMIA MASLAHI YA WATUMISHI

Mwenyekiti wa baraza la wazee wa CCM wilaya ya Makete Mzee Amos Sukunala Nkwama wakati akiongea na waandishi wa habari

Serikali imeshauriwa kusimamia kwa karibu masilahi ya watumishi wakiwemo waalimu, madaktari na wengine ili huduma ziendelee kutolewa kma zilivyotarajiwa kwa wananchi

Rai hiyo imetolewa na baraza la wazee wa chama cha mapinduzi (CCM) wilaya ya Makete kupitia kwa mwenyekiti wake Mzee Amosi Sukunala Nkwama wakati akizungumza na waandhshi wa habari kwenye ofisi za chama hicho wilaya

Pamoja na hayo baraza hilo limeomba sheria ya matibabu bure kwa wazee ifanye kazi kama ilivyopitishwa ili kuwalinda wazee wanapopata maradhi wakati wowote

“Unajua watu wanatusahau sisi wazee na kutudharau kana kwamba hatuwezi kufanya chochote, tukienda hospitalini tunatozwa fedha, wakati hatuna uwezo wa kufanya kazi, lakini ikumbukwe sisi wazee ndio tuliohangaikia huduma hizi tangu zinaanzishwa wakati sisi tukiwa vijana kama wao” alisema Nkwama

Naye Katibu wa CCM wilaya ya Makete Miraji Mtaturu ambaye pia ni katibu wa baraza la wazee ndiye aliyeyasoma maazimio hayo mbele ya waandishi wa habari ambapo yapo maazimio sita

Mbali na hayo ya awali mengine ni kumpongeza mwenyekiti wa Taifa Dkt Jakaya Kikwete kwa kura za kishindo alizopata na kupewa ridhaa ya kuongoza chama kwa miaka kitano ijayo, Kuupongeza mkutano mkuu wa taifa ulivyoendeshwa kwa kuchagua viongozi mahari, wachapakazi na wazalendo kwa chama na chi kwa ujumla, kuupongeza mkutano mkuu kwa namna ulivyofanyika kwa kuonesha dira ya mafanikio katika kuisimamia serikali na kutekeleza wajibu wake kwa wananchi pamoja na kuendelea kuunga mkono juhudi za mwenyekiti wa CCM Taifa kupiga vita ufisadi, uzembe na vurugu za kisiasa zinazopelekea uvunjifu wa amani


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo