ALIYEKUWA MWENYEKITI CCM AWAUMBUA VIONGOZI WAKE KWA UONGO

 Mifuko ya Saruji 24 iliyoharibika
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Mlaguzi, Antony Msagala (CCM) akitoa Tamko la Viongozi wake kusema Uongo na kumdharilisha juu ya Ubadhirifu wa Zahanati 2
---
Bryceson Mathias, Mlaguzi Mvomero
ALIYEKUWA Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Mlaguzi, Antony Damiani Msagala (Gambus) (60) amesema, licha ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kumdhaLilisha na kumfedhehesha,  bado viongozi wake wamejiumbua kwa kusema uongo kuhusu ubadhirifu wa Ujenzi wa Zahanati na kuacha Mifuko ya Saruji 24 ya thamani ya sh. 384,000/-Kuganda.

Msagala alisema hayo akisherehekea Krismas 25.12 ikiwa siku chache  baada ya wananchi wa Mlaguzi kuupiga Chini Uongozi wa watu 17 wa Halmashauri ya Serikali ya CCM akiwemo yeye na Katibu wake Daudi Kikoti aliyefariki ghafla ambapo Idadi kubwa ya wakazi walijiunga na Chama Demokrasia na Maendeleo,

Akizungumza na Mwandishi aliyekuwa akikagua zahanati iliyotolewa taarifa kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero kwamba iko kwenye hatua ya Lenta wakati iko kwenye Msingi wa Magoti (picha zimeambatanishwa - tunazo), Mwenyekiti huyo alisema,

“Nilishangaa Uongozi wa Kata ya Sungaji kutaka niwape Mihutasari ya maamuzi yaliyofanywa na vikao kuhusu mapato na matumizi ya fedha zilizotengwa kwa ajili ya Ujenzi wa Zahanati hiyo, na kinachonisikitisha ni taarifa ya Uongo iliyotolewa ati Ujenzi uko kwenye Lenta wakati iko kwenye Msingi.

Kwenye Kikao halali tuliidhinisha zichukuliwe Benki Mil. 410,000/- sasa kikao kilichoidhinisha Mil. 4.8/- zilizochakachuliwa sijui Mwenyekiti wake alikuwa nani na muhutasari aliupitisha nani mie sihusiki,…lakini hao wanotaka niutoe ule halali tuliopitisha ili wachakachue siwapi labda waniue”.alisema Msagala.

Naye Katibu Mwenezi wa CCM kijijini hapo Method Malishali Clemence Pichani alisema ameamua kujiuzulu Uenezi wa Chama kwa madai hawezi kueneza Uongo maana ni aibu, na akadai kuna mifuko 24 ya saruji iliyoganda ya Laki 384,000/- ambayo ni hasara.

Aidha Viongozi mbalimbali akiwemo Kiongozi wa Dini ya Romani Katoliki (RC) Katekista Emmanuel Gabriel Chambo, Aliyekuwa Mgombea wa Kata ya Sungaji (CHADEMA) Jairos Msigwa, na Diwani Mstaafu wa Kata ya Sungaji Waziri Chamwenye (CCM), walilalamikia Mil. 4.8/- Kati ya Mil.36 za Mradi huo kutumika vibaya, ambapo Katekista Chambo alidai, anasikitishwa anasikitishwa na waumini wanaose Uongo kwa kuwa
hakuna Mchanga au Mawe yaliyonunuliwa ila wananchi walisomaba akiwamo yeye.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo