UVUVI HARAMU ZIWA NYASA UPANDE WA KYELA WAZIDI KUKITHIRI



Na  Ibrahim  Yassin,

IMEELEZWA  kitendo  cha kukithiri  kwa  vitendo  vya  uvuvi  haramu  vinavyo  fanywa  na wavuvi  katika forodha  mbali mbali  katika  ziwa  nyasa  wilayani Kyela Mbeya  ni  moja  ya  sababu  inayoifanya  Halmashauri  ya wilaya hiyo kuigia  kwenye  kashfa  ya  kupuuza  agizo la waziri mkuu  Mizengo  Pinda alilotoa siku za nyuma  akiiagiza wizara  ya maendeleo  ya  mifugo  na  uvuvi  kuhusu  usalimishaji  wa zana haramu za uvuvi,

Wakizungumza  na  waandishi   wa habari akiwemo mwandishi wa  mtandao huu Ibrahim Yassin waliofanya  ziara  ya kushtukiza  kwenye  forodha  hizo  mara baada  ya  kupata taarifa  ya  kuwepo  kwa vitendo vya uvuvi  haramu,baadhi  ya  wakazi  wanaoishi pembezoni mwa  ziwa hilo walidai kuwa wavuvi hao  wamekuwa wakitumia nyavu zilizowekwa  vyandarua katikati  na kuvua dagaa waliokatazwa  kisheria  huku wakiharibu  mazalia  ya  samaki,

Walidai kuwa pamoja na jitihada za maafisa  uvuvi  kufanya doria  mara kwa mara  ya kuwasaka wavuvi hao lakini bado tatizo linaendelea  kuwa sugu,kutokana na uchache wa maafisa hao ukilinganisha na uwingi wa wavuvi na idadi nyingi za forodha zilizopo pembezoni mwa ziwa hilo,

Afisa  uvuvi wa wilaya ya Kyela, Yusuph  Baraka alipoulizwa na wanahabari  kuhusu kukithiri  kwa vitendo vya  uvuvi haramu kwenye ziwa hilo,alikiri kuwepo kwa uvuvi huo na kudai kuwa  wamefanya jitihada  nyingi za kuwadhibiti wavuvi hao lakini zoezi linaonekana kuwa gumu kutokana na uchache wao na pia katika msaka walioufanya  mwishoni  mwa mwezi huu wamefanikiwa kukamata  nyavu 10 zilizowekwa  vyandarua  katikati na nyavu 50 za ngerwa zilizokuwa na macho madogo,

Awali  waziri mkuu Mizengo  Pinda aliiandikia barua wizara hiyo yenye kumbukumbu na pm/p/569  142 ya tarehe 18/01/2010,iliyohusu kusalimisha zana haramu za uvuvi  na  kuitaka sheria ya  uvuvi  ya mwaka 2003 na kanuni zake za  mwaka 2009 zinazoelekeza matumizi  ya  nyavu  za kuvulia  dagaa,

 Barua hiyo  iliandika kuwa ,nyavu zinazotakiwa  kuvulia  dagaa ni zile zenye ukubbwa wa macho yasiyopungua milimita 8 kwenye maji baridi,na milimita 10 kwenye maji chumvi,hatua hiyo ilichukuliwa ili kuhakikisha wingi wa dagaa unaogezeka  kwenye maji hayo na utafiti utakapoonyesha  mabadiliko ya rasilimali hizo kanuni hizo zitabadilika,

Kutokana na agizo hilo la maandishi la waziri mkuu,Halmashauri  ya wilaya ya Kyela imeonekana  wazi  wazi kuwa  imekaidi agizo hilo kutokana na wavuvi wanaotumia ziwa nyasa kuendelea kuvua uvuvi haramu huku wakiharibu mazalia ya samaki kwa  kutumia  nyavu zilizowekwa vyandarau  katikati,

Mkurugenzi  wa Halmashauri ya wilaya ya Kyela ,Clement Kasongo alisema kuwa ni kweli tatizo hilo lipo lakini vijana wake waejitahidi  kufanya doria za mara kwa mara zilizo fanikisha kukamata nyavu 60 zilizo kuwa zikitumika  kuvulia samaki kinyume na taratibu za zilizo wekwa na kuongezwa kuwa operesheni hiyo ni endelevu,

Mwenyekiti  wa Halmashauri   hiyo Gabriel Kipija,kwa upande wake alidhibitisha kuwepo kwa vitendo hivyo  na kudai kuwa  halmashaur yake kupitia  idara ya uvuvi  inakabiliwa na changamoto  kadhaa ikiwapo ya upungufu wa watumishi wa idara hiyo,ukosefu wa boti  speed  kwa ajili ya kufanyia doria majini,na pia watazipeleka changamoto hizo wizara husika ili kuzipatia majibu changamoto hizo.

Unaweza kuwasiliana na mwandishi huyo kwa simu 0653369996,0767269996.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo