SAKATA LA RUSHWA LINALOIKABILI IDARA YA AFYA KYELA LACHUKUA SURA MPYA


Na  Ibrahim  Yassin, Kyela

KUTOKANA  vitendo  vya  rushwa  vinavyodaiwa  kukithiri  kwenye  hospitali  za  Kyela  mkoani  Mbeya vilivyodaiwa  na diwani  kata ya Ipinda Dr,Hunter  Mwakifuna  alipokuwa  akichangia hoja  ya kamati ya afya  elimu  na  maji  kwenye kikao cha  baraza  la  madiwani   akiwatuhumu wa  watumishi  wa  idara  ya  afya  kuomba   rushwa  kwa  wagonjwa  wanaotumia dawa  za ARVs,watumishi  wa idara  hiyo  wapata  mshituko,

Dr,Hunter  Mwakifuna  ambaye  pia  ni  mwenyekiti wa  Chama  cha mapinduzi  wilayani hapa alitoa shutuma hizo  alipokuwa akichangia hoja  ya kamati hiyo iliyowasilishwa  na  Tuhumaini  Ambakisye  kwenye kikao  cha Baraza hilo lililofanyika  juzi  kwenye  ukumbi  wa Community Center,alisema tuhuma dhidi ya watumishi hao ni aibu na zinapaswa  kukomeshwa,

Alisema  kuwa  kwa  muda mrefu madiwani  wamekuwa wakipokea malalamiko mengi kutoka kwa  wagonjwa wanaotumia dawa za kupunguza makali ya virusi vya ukimwi   ARVskuwa baadhi  ya  wahudumu  katika  kitengo hicho kwenye hospitali hizo wanawaomba rushwa ili wawape huduma hiyo  ingawa  hakutoa ushahidi  kuhusiana na tuhuma hizo,

Katika  hatua nyingine  madiwani hao pia walilalamikia kukosekana kwa jokofu la  kuhifadhia maiti kwenye hospitali  hizo  na kuwa kitendo hicho hakiendani na ali halisi ya  wilaya hiyo yenye wasomi wengi  na  watumishi wengi wa ngazi za juu  akiwemo waziri,

Mkurugenzi  mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kyela Clement Kasongo alijibu tuhuma hizo kwa kuwataka madiwani hao wampelekee  ushahidi  wa  kutosha dhidi ya tuhuma hizo  za watumishi wanao daiwa  kutomba rushwa  kwa  wagonjwa hao ili aunde tume ya kuchunguza  tuhuma hizo,

Mwenyekiti  wa  Baraza  la  watu  wanaoishi  na  virusi  vya  Ukimwi (KONGA)wilayani  Kyela  mkoani  mbeya,Julius  Mwalubalile alipohojiwa  na Tanzania daima kuhusiana  na tuhuma hizo zinazohusu  watu  wake  kuombwa  rushwa  na watumishi  wa idara ya afya katika hospitali  hizo pindi waendapo kuchukuwa  dawa za ARVS,alikana  kuwepo  na tuhuma  hizo,

Mwalubalile  alidai  kuwa  yeye ni mwenyekiti  wa  watu  hao  hajawahi  kuletewa taarifa zinazohusu watu wake  kuombwa  rushwa  na kuwa kimsingi kama  tuhuma  hizo zingekuwepo taarifa zingekuja  ofisini  kwake  kwa  maandishi na yeye angezipeleka  kwenye uongozi  wa juu  ili kupatwa   ufumbuzi  wa tatizo hilo,

“Mimi  ni mwenyekiti  wa  baraza hilo hapa wilayani  kama tatizo  hilo  lingekuwepo  ningeletewa  malalamiko  ofisini,na pia idara ya afya  wilayani  hapa  imeweka mpango wa kupeleka dawa za ARVs kwenye zahanati  zilizopo  vijijini ili watu wachukue dawa  hizo kwenye vijiji  vyao,lakini  wagonjwa  hao wanaacha  kuchukua dawa  huko wakiogopa  kunyoshewa  vidole,  wanakimbilia hospitali  ya wilaya kitu ambacho kinaleta msongamono mkubwa  wakati wa  zoezi la ugawaji  wa  dawa hizo”,alisema Mwalubalile,

Mwenyekiti   wa  halmashauri  ya wilaya ya Kyela Gabriel  Kipija kwa upande wake alikana  kuwepo kwa vitendo hivyo vya rushwa kwenye hospitali hizo na kudai  kuwa  kama vitendo hivyo  vipo yeye kama  mwenyekiti  angeletewa  taarifa,wanaodai kuwa vitendo hivyo vipo wamekurupuka  hawajafanya uchunguzi wa kutosha,isipokuwa wanataka umaarufu wa kisiasa,

Kipija  ameitaja changamoto inayoikabili idara hiyo kuwa ni jengo la kutolea dawa za ARVs  kuwa ni dogo  ukilinganisha na idadi  kubwa  ya wagonjwa  wanaokuja kuchukuwa  dawa hizo na kudai kuwa  wapo kwenye mchakato wa kuongeza  jingo ili ilikupanua wigo wa huduma hiyo itakayopunguza  msongamano wa  wagonjwa  wanaofika hospitalini  hapo  kuchukua dawa.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo