WENGI WAJITOKEZA KUHUDHURIA MAZISHI YA ZENAWI

Sifa na salamu zinatolewa juu ya waziri mkuu Meles Zenawi wa Ethiopia aliyeongoza kwa miaka mingi, ambaye anazikwa katika mji mkuu, Addis Ababa.
Mazishi ya Meles Zenawi
Viongozi wa Afrka na kwengineko wamekuwa wakionesha heshima zao pamoja na Rais Paul Kagame wa Rwanda, ambaye alisema Bwana Meles alitumia upeo wake mkubwa kuendeleza Afrika.

Maelfu ya wananchi wa Ethiopia - wengi wao wakiwa wamevaa T-shirt nyeusi zenye picha ya Bwana Meles - wamejaa kwenye medani kuu ya Addis Ababa.

Bwana Meles anasifiwa kuwa aliongoza maendeleo ya Ethiopia, lakini piya alilaumiwa kwa kukiuka haki za kibinaadamu.

Aliyechukua nafasi yake, Hailemaruiam Desalegn, ataongoza nchi hadi uchaguzi wa mwaka wa 2015.

SOURCE:BBC


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo