WASAIDIZI WA KISHERIA WILAYANI MAKETE WAPATIWA MAFUNZO NA LHRC

 Baadhi ya washiriki

 Bi Imelda Urio kutoka kituo cha sheria na haki za binadamu LHRC akitoa mafunzo
 Bw. Ngajilo, mmoja wa wasaidizi wa kisheria

 wasaidizi wa kisheria wakijadili jambo nje ya ukumbi

Wasaidizi wa kisheria kutoka kwenye kata zilizopo wilayani Makete, wanapatiwa mafunzo ya sheria mbalimbali na kituo cha sheria na haki za binadamu (LHRC) kwa lengo la kuzidi kutoa msaada wa kisheria kwa wananchi wa maeneo hayo

Mafunzo hayo ya siku tatu yamefanyika wilayani hapo kwa kuwakutanisha wasaidizi wote wa kisheria waliopo wilayani hapo kwa lengo la kuzidi kuwajengea uwezo wa kisheria

Mkufunzi kutoka kituo cha sheria na haki za binadamu Imelda Urio amewataka wasaidizi hao wa kisheria kuzingatia sheria wanazofundishwa na pia wawe mdsaada mkubwa wa wananchi wanaohitaji msaada wa kisheria

Miongoni mwa sheria walizofundishwa wasaidizi hao hadi hii leo ni pamoja na sheria ya ndoa, sheria ya ajira na mahusiano kazini pamoja na sheria ya ardhi

Wakizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kupatiwa mafunzo hayo, wasaidizi hao wamesema kwa kiasi kikubwa wanapiga hatua na kupata uelewa mkubwa zaidi wa kisheria ambao nao wanautumia kuwapatia msaada wa kisheria wananchi wa maeneo yao

“Unajua watanzania wengi hatufahamu sheria na ndio maana matatizo ya kisheria yanapotukumba tunakuwa hatuna la kufanya, mafunzo haya yanatupa mwanga walau wa kujua wapi pa kuanzia hili ni jambo jema sana, na tunaomba kituo cha sheria na haki za binadamu kiendelee kutoa mafunzo haya hata maeneo mengine hapa nchini”alisema msaidizi wa kisheria Nebart Sigala kutoka kata ya Lupila wilayani Makete

Mafunzo hayo yaliyoanza jana yanatarajiwa kuhitimishwa hapo kesho


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo