WAHAMIAJI HARAMU WAKAMATWA KILIMANJARO


JESHI la Polisi mkoani Kilimanjaro, linawashikilia wahamiaji haramu 10kutoka nchini Ethiopia  kwa tuhuma za kuingia nchini Kinyume cha sheria.

Mbali na wahamiaji hao jeshi hilo pia linawashikilia watu saba kwa tuhuma za kuwasafirish wahamiaji hao katika eneo la kilema pofo na mjohoroni wilayani moshi mkoani hapa.
 
Akitoa taarifa hizo za kukamatwa kwa wahamiaji hao pamoja na watu hao Kaimu kamanda wa polisi mkoani Kilimanjaro Koka  Moita, alisema kuwa septemba sita majira ya saa tisa na nusu usiku katika eneo la Kilema pofo wilayani moshi zilikamatwa pikipiki nne zilizo kuwa zimewapakia wahamiaji haramu wapatao 8.
 
Alisema wahamiaji hao haramua ambao wamebuni mbinu nyingine za kutumia usafiri aina ya bodaboda walikamatwa wakiwa wametokea eneo la Taeakea wilayani Rombo kueleka wilayani Hai ambapo walikuwa wamepanda pikipiki hizo kwa mtindo wa mshikaki.
 
Akizungumzia tukio jingine kamanda Moita alisema kuwa septemba sita majira ya saa tisa na nusu usiku huko katika eneo la Mjohoroni walikamata pikipiki tatu zikiwa zimewabeba wahamiaji wengine sita wakitokea  wilayani Rombo kuelekea wilayani Hai.
 
Alisema kuwa wakati askari wakijaribu kuwatia nguvuni watu hao wahamiaji haramu wane walifanikiwa kutoroka na kufanikiwa kuwakamatwa wahamiaji wawili pamoja na madereva wa bodaboda hizo.
 
Aidha kamanda huyo alisema kuwa madereva wa bodadoda hizo zote waanashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kuwasafirisha wahamaiaji haramu kinyume cha sheri na kwamba watafikishwa mahakamani mara baada ya uchunguzi kukamilika.
 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo