WAZIRI WA UUCHUKUZI AMSIMAMISHA KAZI MKURUGENZI WA MAMLAKA YA BANDARI


Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe.


DAR ES SALAAM,
 
WAZIRI wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe amemsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Ephraim Mgawe  na viongozi wengine watatu kupisha uchunguzi wa tuhuma mbalimbali bandarini hapo.

Wengine waliosimamishwa kazi ni Wasaidizi wake wawili pamoja na Meneja wa Bandari ya Dar es Salaam.

Waziri Mwakyembe alitoa kauli hiyo leo jijini Dar es Salaam alipozungumza na waandishi wa habari baada ya juzi kuwa na kikao cha dharura na viongozi wa mamlaka hiyo.
Alisema kutokana na upungufu waliobaini wameona ni vema viongozi hao wakakaa pembeni na kwamba ameunda kamati ya watu saba watakaochunguza masuala hayo.

Hatua hiyo kusimamishwa kazi kwa viongozi hao ni mwendelezo wa mikakati ya waziri huyo kusafisha uozo katika taasisi mbalimbali kwani hivi karibuni kumsimamisha kazi Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), Paul Chizi na wakurugenzi wanne kutokana na ukiukwaji wa sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma, ambao umetishia uhai wa shirika hilo.

Akizungumza, Mwakyembe alisema nafasi ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TPA inashikiliwa na Mhandisi Madeni Kipande kutoka Wizara ya Ujenzi na kwa nafasi nyingine akasema  wawekwe watu wenye uadilifu.

“Nimeamua kumchukua mtu nje ya bandari kukaini nafasi ya Mkurugenzi Mkuu ili kuondoa wasiwasi, maana angetoka ndani angeshindwa hata kuingia ofisi.

“Najua uamuzi huu utahojiwa, lakini tuendelee kuzumiliana, kwani ukweli haupingwi,” alieleza.

Pamoja na hatua hiyo, alisema ameunda kamati ya watu saba kuchunguza tuhuma  mbalimbali bandarini hapo.

“Wajumbe wa kamati hiyo sitawataja majina, kwa sababu tuna deal na watu wenye hela…hadidu rejea itakiwa na maswali 50,” alisema.

Mbali na kuwasimamisha kazi watumishi  hao, pia alisema ameiagiza bodi ya mamlaka hiyo kuwasimaisha kazi watumishi wa kituo cha kupokea mafuta cha Kurasini (KOJ) ambao ni Meneja, Meneja wa Jet na Injinia wa mafuta wa kituo hicho.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo