WANANCHI WATOLEWA HOFU KUHUSU SENSA MKOANI IRINGA

Mkuu wa mkoa wa Iringa Dkt Christine Ishengoma (wa tatu kushoto) akiwa na waumini wa dini ya Kiislam na wakristo siku alipoandaa futari wakati wa mwezi mtukufu wa ramadhani Ikulu Iringa

MKUU WA MKOA IRINGA MHE. DKT CHRISTINE ISHENGOMA AMESEMA SENSA YA WATU NA MAKAZI INAYOENDELEA HIVI SASA HAPA NCHINI HAINA UHUSIANO WOWOTE NA ITIKADI ZA DINI WALA CHAMA KAMA AMBAVYO BAADHI YA WATU WANAVYODHANI.
MKUU WA MKOA AMETOA KAULI HIYO LEO WAKATI AKIHOJIWA NA MWANDISHI WA MTANDAO HUU WA www.eddymoblaze.blogspot.com FRANCIS GODWIN,AMESEMA LENGO LA SENSA HII INAYOENDELEA NI KUPATA TAKWIMU NA IDADI YA WATU KWA AJILI YA KUPANGA MAENDELEO YA NCHI NA SI VINGINEVYO.
AMEWATOA WITO KWA WANANCHI KUTOA USHIRIKIANO KWA MAKARANI WANAOFIKA KATIKA KAYA ZAO ILI KUIWEZESHA SERIKALI KUPANGA MIPANGO YA MAENDELEO KWA WANANCHI WAKE
AIDHA AMESISITIZA KUWA ENDAPO KUFIKIA KESHO KUNA MWANANCHI ATAKUWA BADO HAJAHESABIWA WATOE TAARIFA KWA VIONGOZI WA VIJIJI AU MTAA ILI WAWEZE KUHESABIWA


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo